»Vyama vya watumiaji wa maji«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/water-users-associations

Muda: 

00:07:43
Imetengenezwa ndani: 
2016

Imetayarishwa na: 

WOCAT

Vyama vya watumiaji wa rasilimali za maji (WRUA) huundwa na watumiaji wa maji, na wamiliki wa ardhi iliyo kando ya mito. Vyama hivyo huundwa kusimamia na kuhifadhi vyanzo vya maji vya pamoja.

Malengo yao makuu ni kupunguza mizozo kuhusu maji, kutoa mgawanyo sawa wa maji, na kulinda mazingira yaliyo kando ya mto, ambao hujulikana kama maeneo ya pwani.

Kuanzisha chama cha watumiaji wa maji

Nchini Kenya, vyama vya WRUA vilianzishwa miaka ya 1990‘s. Vinaanzishwa na jamii zilizo kando ya mito, na vinahakikisha ushiriki mwema wa wanachama katika maamuzi yote ya usimamizi na matumizi ya maji ya mto.

Utatuzi wa Mizozo

Mizozo hutatuliwa kupitia mgawanyo sawa wa rasilimali za maji kati ya watumiaji wa juu ya mto na wa chini. Asilimia 70% ya rasilimali za maji hupewa jamii, halafu 30% huachwa ili kulinda mazingira yaliyo kando ya mto. Ulinzi wa mazingira yaliyo kando ya mto hufanywa kupitia kufunza wanachama kuhusu kuhifadhi mimea iliyopo, pamoja na kupanda miti kwenye ardhi hiyo.

Ulinzi wa kisima hufanywa kwa kujenga ukuta ukizunguka mito ili kudhibiti mmomonyoko wa ardhi na mporomoko wa matope. Uzoefu unaonyesha kwamba mazungumzo kati ya jamii ndio njia bora ya kutatua mizozo.

Manufaa za vyama vya WRUA

Vyama vya WRUA hutoa mgawanyo sawa wa maji, husaidia kutatua mizozo kati ya wadau, na kuboresha usimamizi wa ardhi na maji.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:25Vyama vya watumiaji wa rasilimali za maji (WRUA) huundwa na watumiaji wa maji, na wamiliki wa ardhi iliyo kando ya mito.
00:2602:52Vyama vya WRUA huhakikisha mgawanyo sawa wa rasilimali za maji kati ya watumiaji wa juu ya mto na wa chini.
00:2:5303:23Mizozo hutatuliwa kupitia mgawanyo sawa wa rasilimali za maji kati ya watumiaji wa juu ya mto na wa chini.
03:2404:17Kuunda uwazi kati ya wanachama wote kwa sababu rasilimali zinagawanywa kwa usawa.
04:1804:32Kulinda rasilimali, na kuweka uzio kuzunguka mto.
03:3305:08Ulinzi wa mazingira yaliyokando ya mto hufanywa kupitia kufunza wanachama kuhusu kuwaelimisha.
05:0905:50Ulinzi wa kisima hufanywa kwa kujenga ukuta ukizunguka mito ili kudhibiti mmomonyoko wa ardhi na mporomoko wa matope.
05:5106:08Manufaa za Vyama vya WRUA ni pamoja na; kutoa mgawanyo sawa wa maji, kutatua mizozo kati ya wadau, na kuboresha usimamizi wa ardhi na maji
06:0907:43Muhtasari.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *