»Utengenezaji wa chakula cha kuku kwa bei nafuu, sehemu ya 1«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=Jxfzo9pfTRI

Muda: 

00:11:43
Imetengenezwa ndani: 
2020

Imetayarishwa na: 

AIM Agriculture

Malisho ni nyenzo muhimu sana katika ufugaji wa kuku na ni kigezo kikuu cha mafanikio ya ufugaji wa kuku.

Iwapo una ujuzi kidogo au huna ujuzi wowote kuhusu utengenezaji wa chakula cha kuku, unaweza kutengeneza chakula chenye sumu au chakula cha ubora duni. Hatika hali hii, kuku wa mayai hawatataga kwa wakati sahihi au watataga mayai machache, wakati kuku wa nyama hawatafikia uzito wa soko baada ya wiki 6.

Vijenzi vya malisho ya kuku

Unapotengeneza malisho, vitu vikuu zinazohitajika ni mahindi kwa ajili ya nishati, wishwa wa ngano au mahindi kwa ajili ya fumuele, na soya ambayo hutoa protini. Mbadala pekee ya soya ni ufuta, lakini unashauriwa kutumiwa na watu wa kitaalamu tu kwa sababu una kiwango kikubwa cha mafuta, na hivyo huongeza kiwango cha mafuta kwenye malisho. Malisho haya yakipewa kuku wa mayai, huongeza mafuta mwilini mwa kuku, na hivyo hatataga mayai.

Unapotumia soya kama chanzo cha protini, ikaange au ipike, kwa sababu soya mbichi ina sumu.

Unaweza kutumia mabaki wa alizeti au mabaki ya mbegu za pamba. Iwapo utatumia mabaki ya mbegu za pamba, hakikisha kwamba hazijapakwa dawa, kwa sababu dawa inaweza kusababisha sumu.

Unaweza pia kuongeza dagaa ingawa hazipendekezwi kwa kuku wa mayai kutokana harufu kali ambayo inaweza kupitishwa hadi kwenye mayai. Pia hupunguza muda wa kuhifadhi mayai kwa sababu ya protini nyingi iliyomu.

Mwisho unahitaji chokaa. Ikiwa malisho ni ya kuku wa mayai, unahitaji asilimia 3% ya chokaa, kwa kuku wanaokua unahitaji asilimia 1.5%, na kwa vifaranga unahitaji asilimia 1.3%. Chokaa ni muhimu sana kwa kuku wa mayai.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0001:30Malisho ni kigezo kikuu cha mafanikio ya ufugaji wa kuku.
01:3102:14Iwapo una ujuzi kidogo au huna ujuzi wowote kuhusu utengenezaji wa chakula cha kuku, unaweza kutengeneza chakula chenye sumu au chakula cha ubora duni
02:1504:50Unapotengeneza malisho, vitu vikuu zinazohitajika ni mahindi, wishwa wa ngano na soya.
04:5105:39Unapotumia soya kama chanzo cha protini, ikaange au ipike
05:4007:55Unaweza pia kutumia mabaki wa alizeti au mabaki ya mbegu za pamba.
07:5609:47Unaweza pia kuongeza dagaa ingawa hazipendekezwi kwa kuku wa mayai.
09:4811:43Mwisho unahitaji chokaa.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *