»Ufugaji wa Sungura nchini Kenya«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=rViMQ-_zVLY&t=94s

Muda: 

00:17:43
Imetengenezwa ndani: 
2019

Imetayarishwa na: 

Farm Kenya

Sungura hula mimea mbalimbali. Sungura huhitaji virutubisho kama vile protini, nishati, madini, vitamini na mafuta ili kuwasaidia kukua vizuri.

Wakulima wanapaswa kulisha sungura malisho kama vile, nyasi, mboga kavu na karoti. Sungura wanaweza kulishwa kwa njia mbili: kulishwa kibiashara ambapo sungura hula vyakula vilivyotengenezwa viwandani, nyasi na maji ya kutosha. Nyasi kavu husaidia katika mfumo wa kusaga chakula. Pia hula malisho kama vile, sukumawiki, kabichi, karoti, na majani ya viazi vitamu. Unapotolea sungura mboga za majani acha zikauke ili kuondoa maji. Wakati wa jioni, tolea sungura nyasi za kutosha, maji na virutubisho vingine.

Hatua za kulisha sungura

Sungura wa miezi 3 na zaidi hula takriban gramu 150, sungura mjamzito hula gramu 180 na sungura anayenyonyesha gramu 300 hadi 400 kwa siku. Maji yanafaa kupewa sungura ili kumsaidia kusaga chakula. Mfugaji anapaswa kudumisha usafi na usafi wa vizimba.

Kagua wanyama kila wakati. Sungura mwenye afya huwa amilifu kila wakati, na kinyesi chake ni cha mviringo. Daima shauriana na daktari wa mifugo unapotambua sungura mgonjwa.

Kulisha vibaya

Mboga zenye unyevu husababisha uvimbe wa tumbo la sungura. Sungura hacheui, jambo ambalo linaweza kusababisha kuhara na kifo. Wakulima hawapaswi kulisha sungura kupita kiasi, bali wape virutubishi vinavyohitajika.

Wakati wa kumwachisha kunyonya, usiwalishe sungura kiasi kikubwa cha chakula, protini, mboga, na maji kwani huku kunaweza husababisha uvimbe.

Magonjwa yanayoathiri sungura

Uvimbe wa sikio huzuia masikio na kusababisha kuwashwa, na uchungu kwa sungura. Tumia mafuta ya taa yaliyochanganywa kuwatibu. Upele husababishwa na minyoo, na huathiri pua.

Ugonjwa wa kuhara damu hupitishwa kutoka kwa mama hadi kwa watoto. Tumia viuavijasumu kutibu ugonjwa huu. Nimonia husababishwa na kutokuwa na hewa ya kutosha katika banda la sungura.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0001:17Kulisha sungura.
01:1802:14Kulisha kibiashara.
02:1502:45Faida za kulisha sungura nyasi
02:4603:20Kutumia majani kama chakula cha sungura.
03:2103:51Milisho iliyopendekezwa kwa sungura.
03:5204:30Madhara ya kulisha sungura mboga zenye unyevu.
04:3105:40Changamoto za ulishaji duni kwa sungura.
05:4106:45Dalili na madhara ya ugonjwa wa masikio.
06:4608:15Madhara ya kulisha sungurakupita kiasi.
08:1609:02Kiasi cha malisho kinachohitajika kwa hatua tofauti za sungura.
09:0310:12Kulisha sungura wakati wa kumwachisha kunyonya, na umuhimu wa kudumisha usafi.
10:1311:03Umuhimu wa kutolea sungura maji ya kutosha, na dalili za sungura mwenye afya.
11:0312:30Sababu na aina za magonjwa katika sungura.
12:3113:15Dalili za ugonjwa wa kuhara damu na matibabu yake kwa sungura.
13:1614:46Sababu na njia za kudhibiti nimonia katika sungura.
14:4715:39Matibabu ya uvimbe wa sikio.
15:4016:38Dalili na njia za kudhibiti ugonjwa wa upele.
16:3917:09Kudumisha usafi katika vizimba vya sungura.
17:1017:43Faida za kula nyama ya sungura.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *