»SLM00 Utangulizi«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/slm00-introduction

Muda: 

11:12:22
Imetengenezwa ndani: 
2017

Imetayarishwa na: 

Countrywise Communication, CIS Vrije Universiteit Amsterdam

Usimamizi uendelevu wa ardhi hutoa msingi wa uzalishaji wa mimea, pamoja na kuthibitisha mfumo wa ikolojia, kutunza vyanzo vya maji na viumbe hai.

Usimamizi uendelevu wa ardhi hudhibiti mabadiliko ya hali ya hewa kwa kukamata na kuhifadhi kaboni. Theluthi ya gesi zinazosababisha mabadiliko ya hali ya hewa hutoka kwenye kilimo, na mabadiliko ya matumizi ya ardhi. Mabadiliko ya hali ya hewa yanahusika na uharibifu wa ardhi. Wakulima wanahamasishwa kuwa wabunifu na teknolojia ili kupata suluhisho za mabadiliko haya. Wafadhili hukabili hali hii kwa kuchangia fedha zaidi ili kuboresha usimamizi uendelevu wa ardhi.

Mbunu za usimamizi wa ardhi

Mistari au mitaro ya mawe ni mfumo wa kuvuna maji ya mvua, ambayo hufanywa kwa kuweka mawe kwa ardhi iliyoteremka. Matuta ya Fanya juu husaidia katika uhifadhi wa udongo. Kilimo cha miti ya mgrivea, ambayo ni mti ya umuhimu anuai kinafanywa na wakulima wengi.

Uvunaji wa maji ya mvua yanayotiriri: Maji yanayotiririka kutoka barabarani yanaweza kuvunwa na kutumiwa kukuza mazao. Mbinu ya kufungia wanyama zizini na kutumia samadi yao kutengeneza biogesi ni moja wapo ya mbinu bora za usimamizi wa ardhi.

Mashimo ya Zai hukusanya maji, na yanafanya zaidi yanapoongezwa na mbolea, na kuwekwa kati ya mistari ya mawe. Mbinu ya demi lunes ni rahisi kuanzisha na hutumika kwa kukuza mazao, miti na malisho.

Kilimo cha kutawanya miti muhimu shambani huunda matawi yanayozuia upepo kubeba udongo. Usimamizi wa rutuba ya udongo kwa kutengeneza mashimo ya mbolea oza na kuongeza mbolea za madini kidogo.

Uhuishaji asili wa ardhi kupitia wakulima ni aina ya kilimo inayoruhusu mimea kuchipuka kutokana na mbegu au miti. Uhusiano mzuri kati ya wakulima na wafugaji ambao huwawezesha wote kufaidika. Mifugo hupata malisho, na mimea hupata samadi. Kilimo cha uhifadhi ni kizuri kwa wakulima wadogo.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
01:0102:00Usimamizi uendelevu wa ardhi hudhibiti mabadiliko ya hali ya hewa kwa kukamata na kuhifadhi kaboni.
02:0103:25Mistari au mitaro ya mawe ni mfumo wa kuvuna maji ya mvua, ambayo hufanywa kwa kuweka mawe kwa ardhi iliyoteremka. Matuta ya Fanya juu husaidia katika uhifadhi wa udongo
03:2604:00Kilimo cha miti ya mgrivea, ambayo ni mti ya umuhimu anuai kinafanywa na wakulima wengi. Uvunaji wa maji ya mvua yanayotiririka husaidia katika kukuza mazao
04:0104:40.Zai pits capture run off water.kufungia wanyama zizini na kutumia samadi yao kutengeneza biogesi. Mashimo ya Zai hukusanya maji
04:4105:18Mbinu ya demi hutumika kwa kukuza mazao, miti na malisho. Kilimo cha kutawanya miti muhimu shambani huunda matawi yanayozuia upepo kubeba udongo.
05:1905:51Usimamizi wa rutuba ya udongo kwa kutengeneza mashimo ya mbolea oza na kuongeza mbolea za madini kidogo. Uhuishaji asili wa ardhi kupitia wakulima
05:5206:36Uhusiano mzuri kati ya wakulima na wafugaji ambao huwawezesha wote kufaidika. Kilimo cha uhifadhi ni kizuri kwa wakulima wadogo
06:3707:37Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *