»matumizi salama ya kemikali za kilimo na uvunaji wa majani ya mboga«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=2bphUPzR628&list=PLXyMQiXhVt9q-9EA2h_Np2oTUNrym28lc&index=79

Muda: 

00:11:17
Imetengenezwa ndani: 
2020

Imetayarishwa na: 

Farm Kenya

Ugonjwa wa Covid-19 umeathiri mfumo wa chakula nchini Kenya. Ugonjwa huo umeathiri uazalishaji, ugavi na mahitaji ya chakula.

Usalama wa chakula ni sehemu muhimu ya utoshelevu wa chakula. Wizara ya kilimo inahimiza mbinu bora za kilimo na usalama wa chakula na mboga. Kemikali za kilimo ni bidhaa za zinazotumika kulinda mimea dhidi ya wadudu, na kuboresha ukuaji wao. Kemikali hizi ni pamoja na viuatilifu, viuawadudu, viuakuvu, viuavijasumu na mbolea za madini. Kemikali ni hatari kwa wanadamu, na kwa hivyo chukua tahadhari wakati wa kununua, kushughulikia na kuhifadhi dawa hizo.

Mavazi ya kujikinga

Unapotumia kemikali, vaa surupwenye, gumbuuti, miwani na barakoa. Kisha vaa kofia na hatimaye glavu.

Hakikisha kwamba surupwenye imevaliwa juu ya gumbuuti ili kuepuka kemikali kuingia kwenye miguu. Vaa glavu kwa mikono. Tayarisha kila kifaa kinachohitajika kabla ya kuchanganya dawa. Kuwa na udongo, brashi na ufagio. Pima kipimo cha dawa kilichopendekezwa.

Kuvuna mboga

Uvunaji wa mapema asubuhi ni bora kwa mazao mengi ya mboga, jua linapokuwa kali sana mmea hunyauka.

Tumia kisu kikali ili kuepuka kuharibu mmea. Acha angalau majani 4 kwa kila mmea, kwani mimea hutengeneza chakula kupitia majani. Vuna mara kwa mara, kwani huku kunaweza kusababisha ladha bora ya mboga na kuongeza mavuno.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:50Ugonjwa wa Covid-19 umeathiri mfumo wa chakula nchini Kenya.
00:0500:50Usalama wa chakula ni sehemu muhimu ya utoshelevu wa chakula.
00:5102:05Kemikali za kilimo ni bidhaa za zinazotumika kulinda mimea dhidi ya wadudu, na kuboresha ukuaji wao
02:0602:37Mavazi ya kujikinga: surupwenye, gumbuuti, miwani na barakoa.
02:3804:03Uangalifu wa ziada lazima uchukuliwe katika kuchanganya kemikali.
04:0405:31Pima kipimo cha dawa kilichopendekezwa.
05:3206:26Kuvuna kwa wakati unaofaa kunaweza kuwa na athari kubwa katika mavuno na ubora wa mazao.
06:2707:10Uvunaji wa mapema asubuhi ni bora kwa mazao mengi ya mboga
07:1108:00Tumia kisu kikali ili kuepuka kuharibu mmea.
08:0108:47Acha angalau majani 4 kwa kila mmea, kwani mimea hutengeneza chakula kupitia majani
08:4809:48Vuna mara kwa mara, kwani huku kunaweza kusababisha ladha bora ya mboga na kuongeza mavuno.
09:4911:17Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *