»Kuweka mbolea kwenye mazao ya mboga«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=xJfB5FyKXkI

Muda: 

00:05:26
Imetengenezwa ndani: 
2014

Imetayarishwa na: 

AHR Videos

Mboga ni chanzo muhimu cha virutubisho na madini. Ubora na wingi wa mboga huamuliwa na mbinu ya uzalishaji.

Wakati wa kurutubisha mboga, hakikisha udongo umetayarishwa vyema na umelimwa kwa kina cha sm 20. Mazao huhitaji virutubisho vya kutosha kwa uwiano unaofaa ili kustawi vyema. Hata hivyo, uwekaji wa virutubisho vinavyohitajika hufanywa kwa kupima udongo.

Uchunguzi wa virutubisho

Chukua sampuli za udongo ili kubaini upungufu wa virutubisho kwenye udongo. Tutumia bomba la kipenyo cha sm 2 na urefu wa sm 15 kupata sampuli 40 za udongo. Changanya sampuli pamoja na uchukue sampuli ndogo za 500g ili zipimwe. Kisha pima pH, na ikiwa iko chini ya 6, ongeza gram 250 ya chokaa kwa mitamraba.

Ili kubaini upungufu wa virutubisho kwenye udongo, tumia kifaa cha kupima udongo, au zingatia dalili za upungufu katika mimea iliyopo.

Umuhimu wa Virutubisho

Mimea huhitaji nitrojeni kwa ukuaji, kwa hiyo viwango vya chini vya nitrojeni hutambulika kwa ukuaji uliodumaa, majani hubadilika rangi, majani yaliyokomaa yanaweza kugeuka manjano na kufa kabla ya kukomaa. Fosforasi huhitajika kwa ukuaji wa mizizi na majani, kwa hivyo upungufu wa fosforasi hutambuliwa na majani kugeuka zambarau. Pia upungufu wa potasiamu hutambuliwa na majani kugeuka njano na kahawia.

Kuweka mbolea

Lima udongo kwa kina cha 10cm, tawanya mbolea sawasawa na uichanganye kwenye udongo. Kwa mimea iliyopandikizwa yenye mizizi ya pembeni, weka mbolea pande zote mbili za mahali ambapo mimea imepandwa. Dumisha afya ya mimea kwa kuongeza NPK na samadi ya mifugo kila baada ya wiki 2–4.

Upe udongo kinachohitajika kwa tija ya juu.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:38Wakati wa kurutubisha mboga, hakikisha udongo umetayarishwa vyema na umelimwa kwa kina
00:3901:14Chukua sampuli 40 za udongo ili kubaini upungufu wa virutubisho kwenye udongo.
01:1502:07Pima pH ya udongo, ikiwa iko chini ya 6, ongeza chokaa.
02:0802:33Tumia kifaa cha kupima udongo, au zingatia dalili za upungufu katika mimea iliyopo.
02:3403:16Mimea huhitaji nitrojeni kwa ukuaji. Fosforasi huhitajika kwa ukuaji wa mizizi.
03:1703:29Upungufu wa potasiamu hutambuliwa na majani kugeuka njano na kahawia.
03:3003:53Dumisha afya ya mimea kwa kuongeza NPK na samadi ya mifugo
03:5404:13Lima udongo kwa kina cha 10cm, tawanya mbolea sawasawa na uichanganye kwenye udongo.
04:1404:35Kwa mimea iliyopandikizwa yenye mizizi ya pembeni, weka mbolea pande zote mbili za mahali ambapo mimea imepandwa.
04:3605:00Dumisha afya ya mimea kwa kuongeza NPK na samadi ya mifugo kila baada ya wiki 2–4.
05:0105:17Upe udongo kinachohitajika kwa tija ya juu.
05:1805:26Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *