»Kuvuna na kuhifadhi ufuta«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/harvesting-and-storing-sesame

Muda: 

00:09:00
Imetengenezwa ndani: 
2016

Imetayarishwa na: 

MOBIOM

Ufuta ni rahisi kukuza, lakini mbinu duni za kuvuna, kupura na kuhifadhi zinaweza kupunguza ubora wake. Mawe, changarawe na taka nyingine zinaweza kuchanganyika na mbegu za ufuta na hivyo kuathiri bei.

Ufuta ukikomaa sana shambani, maganda hupasuka na kuachilia mbegu. Ufuta huwa tayari kuvunwa wakati mabua au mashina yanakuwa manjano, majani huanza kudondoka na vifuko vya chini hubadilika kahawia.

Kushughulikia ufuta

Siku chache kabla ya kuvuna, andaa eneo la kukaushia sakafuni au katika kiwanja kilichokaribu. Lazima eneo hilo liwe safi, kavu na lilindwe dhidi ya wadudu na wanyama waharibifu. Eneo la kukaushia linaweza kutengenezwa kwa kuchanganya kinyesi cha ng‘ombe, udongo laini, chumvi na maji. Samadi ya ngombe na udongo hufanya ardhi kuwa ngumu, chumvi huzuia chungu na mchwa kushambulia ufuta. Mabunda ya ufuta pia yanaweza kukaushwa juu ya paa za nyumba ili kuzuia wanyama wasiharibu mbegu.

Kuvuna ufuta

Kabla ya kuvuna, nuwa ringa au kisu cha kuvunia ili kurahisisha uvunaji. Wakati wa kuvuna, kata mabua ya ufuta 10cm juu ya ardhi lakini usitikise mabua kwa sababu mbegu zitadondoka chini. Baada ya kuvuna, acha mabunda shambani kwa masaa kadhaa.

Kusanya mabunda na uyapeleke katika eneo la kukaushia. Fanya mabunda kwa kusimamisha wima mimea uliyokatwa huku vifuko vya mbegu vikiangalia juu.

Kupura na kusafisha mbegu

Pura ufuta wako angalau siku 15 baada ya kukausha kwenye turubai au damani ya plastiki. Huku kunafanywa kwa kutikisa mashina ya ufuta kwa mikono au kutumia kijiti.

Chuja mbegu kupitia vichujio viwili tofauti ili kuondoa mawe, takataka ya mimea na vumbi, na baada ya hapo pepete mbegu na uziweke kwenye magunia safi yaliyoshonwa vizuri.

Hifadhi mbegu kwenye eneo safi lisilopenyeza mvua, na lina hewa ya kutosha. Weka magunia ya ufuta juu ya mbao au magogo ambapo hawagusi ardhi moja kwa moja ili kulinda ufuta dhidi na unyevu.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0001:14Ufuta ni rahisi kukuza, lakini mbinu duni za kuvuna, kupura na kuhifadhi zinaweza kupunguza ubora wake.
01:1502:14Ufuta huwa tayari kuvunwa wakati mabua au mashina yanakuwa manjano, majani huanza kudondoka na vifuko vya chini hubadilika kahawia. Ufuta ukikomaa sana shambani, maganda hupasuka na kuachilia mbegu.
02:1502:27Siku chache kabla ya kuvuna, andaa eneo la kukaushia. Lazima eneo hilo liwe safi, kavu na lilindwe dhidi ya wadudu na wanyama waharibifu
02:2803:10Eneo la kukaushia linaweza kutengenezwa kwa kuchanganya kinyesi cha ng‘ombe, udongo laini, chumvi na maji.
03:1104:20Ufuta pia unaweza kukaushwa juu ya paa za nyumba ili kuzuia wanyama wasiharibu mbegu. Nuwa ringa au kisu kabla ya kuvuna,
04:2104:38Kata mabua ya ufuta 10cm juu ya ardhi lakini usitikise mabua
04:3905:28Kusanya mabunda na uyapeleke katika eneo la kukaushia.
05:2906:21Pura ufuta wako angalau siku 15 baada ya kukaushia kwenye turubai au damani ya plastiki
06:2206:40Chuja mbegu kupitia vichujio viwili tofauti ili kuondoa mawe, takataka ya mimea na vumbi. Pepete mbegu
06:4107:40Weka mbegu kwenye magunia safi yaliyoshonwa vizuri. Weka magunia juu ya mbao au magogo ambapo hawagusi ardhi.
07:4109:00Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *