»Kutenganisha mbegu kwa njia ya kuzifanya kuelea juu ya maji«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/node/3432

Muda: 

00:06:37
Imetengenezwa ndani: 
2016

Imetayarishwa na: 

Agro-Insight, CABI, Countrywise Communication, IRRI, RDA, TMSS

Wakulima huhifadhi mbegu zao kwa msimu ujao, lakini maranyingi mbegu hizo huwa ni za hali ya chini kutokana na madhara ya madudu na magonjwa. Kwa hivyo kuelea mbegu ili kuondoa zilizoharibika huhakikisha kwamba mbegu zako zinatumika.

Kuboresha mbegu ni muhimu ikiwa unataka kuzitumia msimu ujao. Ni muhimu kuanza muzalishaji na mbegu zenye afya. Unajua kwamba mbegu zako zimeshambuliwa, unapofungua chombo kabla ya kupanda na kuona nondo wakitoka ndani na kuruka nje. Pia mashimo madogo ya wadudu yanaonekana. Mbegu zilizoshambuliwa au ambazo hazijakomaa kawaida ni nyepesi kuliko mbegu zenye afya, na kwa hivyo ni rahisi kuziondoa.

Kutenganisha mbegu nzuri kwa mbaya

Safisha mbegu kwa kupepeta. Wakati huu unaweza kuondoa mbegu zozote zilizo na mashimo. Baadaye unaweza kuweka mbegu kwenye maji ili uone ni mbegu gani; ambazo hazijajazwa, vumbi, magada amabayo hayana mbegu ndani, na majani. Sio zote zilizoathiriwa zinaweza kuonekana na kutenganisha kwa kuzitia tu ndani ya maji.

Ili kuondoa mbegu zote mbovu, ni dhahiri kuongeza uzito wa maji. Kwanza, Jaza mtungi safi na maji. Kisha ongeza chumvi na urea halafu uchanganye. Unajua umeongeza chumvi na urea vya kutosha, wakati utakapoona kwamba yai linaelea juu ya maji. Weka mbegu kwenye mchanganyiko na ukoroge kwa mikono. Baada ya muda mchache,utaona mbegu zote mbovu zikielea juu ya maji. Mbegu nzuri zitabaki chini ya mtungi. Ondoa mbegu mbovu yote na uwape kuku wako. Kisha ondoa mbegu nzuri, na lazima zioshwe mara mbili hadi tatu ukitumia maji safi.

Unaweza kuacha maji ya chumvi kwenye chombo tofauti na utumie kunyunyizia miti ya mnazi. Ikiwa maji ni mchanganyiko wa urea, unaweza kuitumia kwa kitalu.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:26Utangulizi
00:2700:40Wakulima huhifadhi mbegu zao kwa msimu ujao, lakini maranyingi mbegu hizo huwa ni za hali ya chini kutokana na madhara ya madudu na magonjwa
00:4100:46Attacked or unripe seeds are usually lighter than healthy seeds and therefore easy to get rid of.
00:4701:16Unajua kwamba mbegu zako zimeshambuliwa, unapofungua chombo kabla ya kupanda na kuona nondo wakitoka ndani na kuruka nje
01:1701:22Safisha mbegu kwa kupepeta
01:2302:30Kisha, uweka mbegu kwenye maji ili uone ni mbegu gani ambazo hazijajazwa, vumbi, na magada.
02:3102:53Jaza mtungi safi na maji
02:5402:59Kisha ongeza chumvi na urea
03:0003:08Unajua umeongeza chumvi na urea vya kutosha, wakati utakapoona kwamba yai linaelea juu ya maji
03:0903:19Weka mbegu kwenye mchanganyiko na ukoroge kwa mikono
03:2003:26Mbegu mbovu zote zitaelea juu ya maji
03:2703:38Mbegu nzuri zitabaki chini ya mtungi.
03:3903:50Unaweza kuacha maji ya chumvi kwenye chombo tofauti
03:5104:04Lazima zioshwe mbegu nzuri mara mbili hadi tatu ukitumia maji safi.
04:0504:14Ondoa mbegu mbovu yote na uwape kuku wako
04:1505:25Tumie maji ya chumvi kunyunyizia miti ya mnazi. Ikiwa maji ni mchanganyiko wa urea, unaweza kuitumia kwa kitalu.
05:2606:15Muhtasari
06:1606:37Credits

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *