»Kupandikiza pilipili«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/transplanting-chillies

Muda: 

00:11:35
Imetengenezwa ndani: 
2016

Imetayarishwa na: 

Agro-Insight

Shamba nzuri la pilipili huanza kwa miche thabiti yenye afya. Hii inaweza kufanyika kwa kuandaa kitalu kizuri, kuandaa shamba vizuri na kushughulikia miche wakati wa kupandikiza.

Ili kukuza miche ya pilipili yenye ubora mzuri katika kitalu, unafaa kurutubisha na kulainisha udongo, na kumwagilia maji ya kutosha. Andaa kitalu kiwe cha upana wa mita 1, na karibu na shamba ili iwe rahisi kupandikiza miche. Panda mbegu chache tu kwa kila mtaro.

Kanuni au miongoza ya kupandikiza

Andaa shamba mapema kwa kuondoa magugu na kulainisha udongo. Kisha ongeza mboji au mbolea, kwani pilipili hukua vyema kwenye udongo laini, uliyo na rutuba.

Pandikiza wakati miche ina nguvu ya kutosha kujisimamisha yenyewe, lakini usiiache ikae kwenye kitalu kwa muda mrefu. Kuacha nafasi kati ya mimea hutegemea tabia ya ukuaji wa pilipili. Aina inayomea wima inafaa kupandwa kwa mwachano wa 40cm kwa 40cm, na mwachano wa 40cm kwa 80cm kwa aina inayotambaa.

Pandikiza miche jioni. Mwagilia maji kitalu kabla ya kupandikiza ili iwe rahisi kuondoa miche bila kuiharibu.

Unapopanda, punguza mizizi ya miche ikiwa ndefu sana ili mimea istawi vizuri. Panda mche mmoja katika kila shimo kwa kina cha takribani 5cm. Hakikisha kwamba unapandikiza kwa uangalifu.

Baada ya kupandikiza, miche hunyauka kidogo, na hii ni kawaida. Mwagilia miche maji ili iweze kustawi.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:22Shamba nzuri la pilipili huanza kwa miche thabiti yenye afya
00:2300:57Kuandaa shamba na kupandikiza huathiri uhai wa miche shambani.
00:5801:59Udongo tifutifu uliyo na rutuba ni bora kwa kukuza pilipili. Pata mbolea ya kikaboni mapema.
02:0002:11Ua mbegu za magugu zilizo kwenye kinyesi cha ng‘ombe kwa kuoza.
02:1202:26Andaa kitalu kiwe cha upana wa mita 1, na karibu na shamba
02:2702:48Kwa miche yenye afya na nguvu, lazima udongo uwe na rutuba, laini na maji. Usipande mbegu nyingi kwa mtaro mmoja.
02:4903:48Pandikiza wakati miche ina nguvu ya kutosha
03:4904:20Fanya maandalizi ya shamba mapema, ukiongeza mboji / mbolea oza.
04:2104:51Mwagilia maji mara tatu kabla na baada ya kupandikiza katika wakati wa kiangazi.
04:5205:32Kuacha nafasi hutegemea tabia ya ukuaji wa aina ya pilipili
05:3306:49Andaa mashimo ya kupanda kwa kutumia vijiti au kamba
06:5007:17Pandikiza jioni kwenye udongo uliyo na unyevu.
07:1807:31Unapopanda, punguza mizizi ya miche ikiwa ndefu sana ili mimea istawi vizuri.
07:3207:49Tunza miche kwa uangalifu wakati upandikiza.
07:5008:59Panda mche mmoja katika kila shimo kwa kina cha takribani 5cm. Hakikisha mzizi mkuu umesimama wima ardhini.
09:0009:21Baada ya kupandikiza, miche hunyauka kidogo, na hii ni kawaida
09:2209:49Katika udongo wa kichanga, weka samadi kwa kila shimo badala ya shamba lote.
09:5011:35Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *