»Kupandikiza /kuatika mpunga«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/node/3423

Muda: 

00:14:16
Imetengenezwa ndani: 
2016

Imetayarishwa na: 

AfricaRice, Agro-Insight, IER, Intercooperation, Jekassy

Ukipanda mpunga kwa kuatika au kupandikiza, waweza kupata mavuno zaidi na udhibiti bora wa magugu. Kwa hivyo usimamizi wa zao lako huwa rahisi.

Ukitawanya mbegu, magugu hutatiza sana. Unapopandikiza au kuatika miche ya mpunga, mavuno yatakuwa bora mara mbili hadi tatu zaidi. Kwa kuongezea unahitaji mbegu chache, kwa hivyo una uwezo wa kuchagua miche za hali ya juu. Mpunga huzaa zaidi, wakati kuna matawi zaidi, kwa sababu kila tawi hutoa wimbi. Kutoa matawi kunategemea na umri wa miche, kina cha kutoa matawi na umbali kati ya mimea.

Jinsi ya kuatika/ kupandikiza

Tumia miche mizuri, lakini hakikisha hujatumia mingi sana kwenye kitalu, kwa sababu utapata miche zilizokonda na dhaifu. Miche zinafaa kuwa na majani manne na kupandikizwa takriban siku 15 hadi 20 baada ya kupanda. Ikiwa miche zina majani matatu tu, hazitaki kina kirefu unapoziatika. Miche zilizo komaa zaidi zina matawi kidogo na zinahitaji muda mrefu kabla ya kuanza kumea.

Sawazisha shamba lako na kukanda udongo ili kurahisisha kuatika miche. Hakikisha kuna kiwango kidogo cha maji shambani siku chache kabla ya kuatika. Ni dhahiri Shamba liwe tayari kabla ya miche ndani ya kitalu hazijakaa wiki mbili. Kabla ya kung‘oa miche unafaa kumwagilia maji ili kupunguza uharibifu kwa mimea. Ziatike haraka uwezekanavyo, ili kuzuia miche kunyauka.

Weka sehemu ya chini ya mche iliyonyeupe kwenye tope, na acha sehemu ya kijani juu ya ardhi. Miche itakua polepole, wakati sehemu ya kijani iko chini ya ardhi. Kukua kwa mimea kutaathiriwa sana iwapo hiyo sehemu ya kijani kibichi itawekwa kwenye udongo. Mizizi ikipandwa kwa kina kirefu, hukosa hewa safi ya oksijeni, hutoa matawi kidogo na itafariki.

Miche za mpunga zinahitaji nafasi ili kunawiri na kutoa matawi. Kwa hivyo unafaa kuongeza miche moja hadi tatu kwa kila kilima cha upanzi. Wakati wimbi linapoanza kuchipuka, matawi huacha kukua na mwavuli huwa unafungwa. Kwa hivyo mpunga huzaa zaidi na una magugu machache.

Pandikiza/ atika mpunga kila baada ya sentimita 20. Wakulima wengine hutumia kamba baada ya kila sentimita 20. Unaweza pia kuweka alama kwa kijiti au kutumia miguu, ama mikono ili kupata vipimo halisi vya kupanda miche. Unafaa kusawazisha vipimo kati ya miche. Ukipanda miche katika mistari itakuwa rahisi kuondoa magugu. Miche zikifariki katika harakati za kuatika, basi zipande upya chini ya muda wa wiki moja.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0001:51Utangulizi
01:5202:39Ukitawanya mbegu, magugu hutatiza sana
02:4002:57Unapopandikiza au kuatika miche ya mpunga, mavuno yatakuwa bora mara mbili hadi tatu zaidi
02:5803:05Unahitaji mbegu chache, kwa hivyo una uwezo wa kuchagua miche za hali ya juu.
03:0603:21Ukipanda mpunga kwa kuatika au kupandikiza, waweza kupata mavuno zaidi na udhibiti bora wa magugu
03:2204:22Tumia miche mizuri, lakini hakikisha hujatumia mingi sana kwenye kitalu, kwa sababu utapata miche zilizokonda na dhaifu.
04:2305:29Miche zinafaa kuwa na majani manne na kupandikizwa takriban siku 15 hadi 20 baada ya kupanda.
05:3006:01Ikiwa miche zina majani matatu tu, hazitaki kina kirefu unapoziatika
06:0206:26Sawazisha shamba lako na kukanda udongo ili kurahisisha kuatika miche
06:2706:34Ni dhahiri Shamba liwe tayari kabla ya miche ndani ya kitalu hazijakaa wiki mbili.
06:3506:48Kabla ya kung‘oa miche unafaa kumwagilia maji ili kupunguza uharibifu kwa mimea.
06:4906:55Atike mimea kwa haraka uwezekanavyo, ili kuzuia miche kunyauka.
06:5608:10Weka sehemu ya chini ya mche kwenye tope, na acha sehemu ya kijani juu ya ardhi.
08:1108:46Mizizi ikipandwa kwa kina kirefu, hukosa hewa safi ya oksijeni, hutoa matawi kidogo na itafariki.
08:4709:44Miche za mpunga zinahitaji nafasi ili kunawiri na kutoa matawi. Kwa hivyo unafaa kuongeza miche moja hadi tatu kwa kila kilima cha upanzi
09:4510:29Wakati wimbi linapoanza kuchipuka, matawi huacha kukua na mwavuli huwa unafungwa.
10:3011:02Wakulima wengine hutumia kamba baada ya kila sentimita 20.
11:0311:20Unaweza pia kuweka alama kwa kijiti au kutumia miguu, ama mikono ili kupata vipimo halisi vya kupanda miche
11:2111:47Ukipanda miche katika mistari itakuwa rahisi kuondoa magugu.
11:4813:38Muhtasari
13:3914:16Credits

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *