»Kukuza miche bora ya bamia«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/making-good-okra-seeding

Muda: 

00:12:16
Imetengenezwa ndani: 
2019

Imetayarishwa na: 

Alcide Agbangla

Bamia hupandwa moja kwa moja kutoka kwa mbegu, lakini kupanda mbegu nyingi katika kila shimo hupunguza ukuaji, na mavuno. Ili kupata miche mizuri ya bamia, tumia mbegu bora na mbinu bora za usimamizi.

Kupata mbegu bora

Unaweza kupata mbegu bora kwa kununua mbegu zilizoboreshwa au mbegu aina za kienyeji. Ili kupata mbegu kutoka kwa aina za kienyeji, tambua mimea yenye mashina kubwa na thabiti, na uvune mbegu za matunda makubwa. Kabla ya matunda yaliyoiva kuanguka, basi fungua matunda na uchague mbegu kubwa, zisizo na uharibifu wala kasoro. Baada ya kuzipata mbegu, zikaushe kivulini kwenye eneo safi la kukaushia, na uzihifadhi katika chombo kisichopenyeza hewa wala unyevu na mwanga wa jua.

Mbinu za shambani

Bamia hukua katika kila aina ya udongo hata bila mbolea, na inaweza kupandwa katika shamba, au vitalu vilivyoinuliwa kwa kuacha nafasi ya umbali na upana wa 40x 80cm. Ili kupata mavuno bora, anzisha shamba lako kwenye jua, na ufanye kilimo cha kwanza ili kufungua na kutifua udongo. Kabla ya kupanda, mbegu zinaweza kuoteshwa, kisha ndio mbegu 2–3 zipandwe kwa kila shimo la kina cha 2cm na kufunikwa na udongo. Ikiwa bamia zimepandwa kwenye vitalu, mwagilia maji baada ya kupanda. Tandaza shamba baada ya mimea kunawiri.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:36Bamia hupandwa moja kwa moja kutoka kwa mbegu
00:3701:22kupanda mbegu nyingi katika kila shimo hupunguza ukuaji, na mavuno. Panda mbegu bora.
01:2301:54Tambua mimea, na uvune mbegu kutoka kwa matunda thabiti na makubwa. Kabla ya matunda yaliyoiva kuanguka
01:5502:14Fungua matunda na uchague mbegu kubwa, kisha zikaushe.
02:1502:54Zihifadhi katika chombo kisichopenyeza hewa wala unyevu na mwanga wa jua.
02:5503:23Bamia hukua katika kila aina ya udongo hata bila mbolea. Anzisha shamba lako kwenye jua.
03:4004:39Fanya kilimo cha kwanza kabla ya kupanda, na palilia shamba vizuri. Tumia nyaasi kama matandazo.
04:4006:15Bamia inaweza kupandwa katika shamba, au vitalu vilivyoinuliwa kwa kuacha nafasi ya umbali na upana wa 40x 80cm
06:1606:44Acha nafasi kati ya kila safu au mustari, na kati ya vitalu.
06:4508:26Mbegu za bamia huhitaji unyevu kukua vyema. Mbegu zinaweza kuoteshwa kabla ya kupanda.
08:2710:02Panda mbegu 2–3 katika kila shimo la kina cha 2cm, na zifunike kwa udongo.
10:0310:21Ikiwa bamia zimepandwa kwenye vitalu, mwagilia maji baada ya kupanda.
10:2212:16Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *