“ Kudhibiti magonjwa ya vitunguu“

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/managing-onion-diseases

Muda: 

00:11:15
Imetengenezwa ndani: 
2016

Imetayarishwa na: 

Agro-Insight

Vitunguu hukua vizuri katika mazingira tofauti. Vitunguu hupata magonjwa zaidi wakati wa joto na unyevu. Magonjwa husambazwa na udongo, mbegu au mabaki yaliyoathiriwa.

Dalili za magonjwa ya vitunguu ni madoa ya hudhurungi, mistari ya manjano na majani kujikunja. Ili kukuza vitunguu vyenye afya, panda aina bora za mbegu kwa kutafuta ushauri kutoka kwa washauri. Nunua mbegu zilizotibiwa kutoka kwa wauzaji wanaoaminika ili kuepuka miche yenye ubora duni.

Kuzuia magonjwa

Ongeza mbolea oza kwenye kitalu ili kudumisha vitunguu vyenye afya na sugu dhidi ya magonjwa. Panda mbegu kwa mstari na acha nafasi ya kutosha ili kuwezesha upitaji mzuri wa hewa. Ondoa miche yenye magonjwa na dhaifu wakati wa kupandikiza ili kuzuia kuenea kwa magonjwa. Inua vitalu hasa wakati wa masika ili kuwezesha kutoa maji ya ziada kwa urahisi. Mwagilia maji ya kutosha, lakini epuka kumwagilia maji mengi sana. Daima, nyuyizia maji mimea asubuhi ili iwe na muda wa kukauka wakati wa mchana. Palilia mara kwa mara ili kusababisha mzunguko mzuri wa hewa.

Kukagua shamba kila wakati ni muhimu ili kutambua kwa urahisi mimea iliyoathiriwa na magonjwa. Ng‘oa vitunguu vilivyo na ugonjwa na uvizike ili kudhibiti kuenea.

Tumia mbolea za majani ili kukuza mimea thabiti, yenye afya. Tumia dawa za kuua kuvu ili kuzuia magonjwa.

Fanya mzunguko wa mazao ili kuangamiza ugonjwa. Usipande vitunguu kwenye shamba lenye ugonjwa kwa miaka 3. Ondoa mabaki ya mimea baada ya kuvuna ili kuzuia kuambukizwa tena.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:40Vitunguu hupata magonjwa zaidi katika msimu wa mvua.
00:4101:02Vitunguu hupata magonjwa zaidi wakati wa joto na unyevu, na mahali ambapo maji hukusanyika.
01:0301:26Dalili za magonjwa ya vitunguu:
01:2701:43Madoa ya hudhurungi, mistari ya manjano na majani kujikunja.
01:4401:51Jinsi ya kuzuia na kudhibiti magonjwa.
01:5202:26Fanya mzunguko wa mazao.
02:2703:01Panda mbegu zilizoboreshwa.
03:0203:30Nunua mbegu zilizotibiwa kutoka kwa wauzaji wanaoaminika.
03:3103:45Ongeza mbolea oza kwenye kitalu ili kudumisha vitunguu vyenye afya.
03:4603:59Inua vitalu hasa wakati kupanda
04:0004:36Panda mbegu kwa mstari na acha nafasi ya kutosha
04:3704:50Ondoa miche yenye magonjwa na dhaifu wakati wa kupandikiza.
04:5105:09Mwagilia maji ya kutosha.
05:1005:26Daima, nyuyizia maji mimea asubuhi.
05:2705:40Palilia shamba mara kwa mara
05:4105:48Kagua shamba mara kwa mara.
05:4906:15Ng‘oa vitunguu vilivyo na ugonjwa na uvizike.
06:1606:50Tumia mbolea za majani.
06:5107:30Tumia dawa mbalimbali za kuua kuvu.
07:3108:29Tumia viuatilifu vya asili.
08:3008:44Ondoa mabaki ya mimea baada ya kuvuna.
08:4511:15Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *