Kwa kuwa ni zao la lishe bora, mahitaji ya nyanya sokoni huongezeka mara kwa mara. Ila, nyanya huwa hazitoshi sokoni kutokana na uzalishaji duni unaosababishwa na mbinu duni za kilimo zinazotumika.
Ili kupanda nyanya unahitaji kuchukua mbinu bora za uzalishaji kama vile kutumia aina bora, kuzingatia msimu wa kupandia, na njia ya kupanda. Wakati wa kupanda, acha nafasi ambayo husaidia katika uingizaji wa hewa, umwagiliaji wa maji, na kuondoa maji ya ziada.
Kupanda nyanya
Kwanza, tawanya kilo 8 za NPK na kilo 3 za mbolea ya kikaboni kila baada ya mita 2 katika kitalu. Tayarisha miche ya mimea, na upande mimea 26600 kwa hekta. Panda kwa kina kinachofaa na kisha funika miche. Mwagilia maji kwa upole, weka trei kwenye kitalu kilicho na unyevu wa kutosha na hewa.
Baada ya siku 4 hadi 7 ondoa kivuli na punguza umwagiliaji wa maji ili kufanya miche iwe migumu. Pandikiza miche baada ya siku 28, kwa kina kinachofaa na muachano wa 50cm. Endelea kumwagilia maji, na andaa nafasi pa kuwezesha mimea kutambaa wiki 2 baada ya kupandikiza.
Kwa mavuno bora, kuna haja ya kufanya mashauriano, kuweka mbolea, kufuata mapendekezo, kukagua shamba na kuondoa mimea iliyoambukizwa.
Kuvuna nyanya
Uvunaji hufanyika ndani ya siku 60 hadi 70 baada ya kupandikiza, wakati wa asubuhi au alasiri. mavuno huwekwa kwenye eneo lililo na kivuli na hewa ya kutosha.