»Hatua sita za kuvuna zaidi ya tani 20 za muhogo kwa hekta moja«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=4vWLz6EbQO8

Muda: 

00:04:14
Imetengenezwa ndani: 
2019

Imetayarishwa na: 

Cassava Matters

Muhogo ni zao muhimu katika jamii nyingi barani Afrika, lakini mavuno yake kwa ujumla ni madogo. Baadhi ya hatua zinaweza kufuatwa wakati wa ukuzaji wa muhogo ili kuongeza mavuno.

Ili kupata mavuno mengi ya muhogo, chagua eneo linalofaa ambalo halipo kwenye mteremko, halina maji mengi, mawe au lenye kina kifupi sana. Andaa shamba kwa kufyeka na kata vichaka, au kulima iwapo vichaka ni vingi sana. Unaweza pia kufyeka nyasi na magugu ya kudumu na kisha usubiri kwa wiki 2 hadi mimea itakapokufa. Weka dawa ya glyphosate kwenye nyasi zinazochipuka tena. Glyphosate pia inaweza kutumika kwenye shamba lenye nyasi zisizozidi mita moja kwa urefu.

Maandalizi ya ardhi

Kutayarisha shamba kwa ukuzaji wa mihogo, lima ardhi. Gharama za kulima ni kubwa lakini husababisha mavuno mengi. Kulima huongeza mavuno kwa angalau tani 5 kwa ekari. Kutengeneza matuta pia kunaweza kufanywa kwa sababu huongeza mavuno kwa angalau tani 4 kwa ekari. Huku kunapendekezwa iwapo udongo ni wa mfinyanzi mwingi au unapopanga kuvuna wakati wa kiangazi. Baada ya maandalizi ya ardhi, panda mihogo.

Kupanda na kudhibiti magugu

Panda muhogo wakati udongo unapokuwa na unyevu. Panda kwa umbali wa mita 1 kati ya safu na mita 0.8 ndani ya safu, kisha weka dawa ya kuua magugu baada ya kuibuka.

Wakati magugu yanapofunika asilimia 3o% ya shamba au mihogo inapofikia hatua ya majani 4 hadi 6, kutumia dawa za kuua magugu, palizi kwa mitambo au kwa mikono. Unapotumia dawa ya kuua magugu, weka kizuizi kwenye kinyunyizio ili kuzuia dawa kugusa sehemu za kijani za muhogo. Usitumie dawa ile ile ya kuua magugu mwaka baada ya mwaka, kwani hii inaweza kusababisha ukuaji wa magugu sugu.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:20Chagua eneo linalofaa
00:2100:34Ikiwa mimea ni mirefu sana, nyunyizia dawa za kuua magugu, kwanza fyeka mimea na kisha ulime.
00:3501:20Fyeka nyasi na magugu ya kudumu na kisha usubiri kwa wiki 2 ndio uweke glyphosate.
01:2102:07Lima ardhi. Kuweka matuta kunapendekezwa ikiwa udongo una kiwango cha juu cha udongo wa mfinyanzi, au ikiwa unapanga kuvuna wakati wa kiangazi.
02:0802:43Panda muhogo udongo unapokuwa na unyevu, kwa umbali wa mita 1 kati ya safu na mita 0.8 ndani ya safu.
02:4403:52Wakati magugu yanapofunika zaidi ya 30% ya shamba lako, tumia mkakati wa kudhibiti magugu kwa kunyunyizia dawa.
03:5304:03Usitumie dawa ile ile ya kuua magugu mwaka baada ya mwaka
04:0404:14Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *