»Pata pesa kwa urahisi kwa kujifunza jinsi ya kutunza kuku wa kienyeji (sehemu ya 1)«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=Q6abe4kgTh8

Muda: 

00:09:40
Imetengenezwa ndani: 
2019

Imetayarishwa na: 

AfriChic

Kuku ni chanzo cha protini na kipato kwa wafugaji, hata hivyo ugonjwa wa kideri huwaangamiza ndege haraka. Kwa hivyo utunzaji mzuri na kufuata hatua zinazopendekezwa unahitajika.

Kinyesi cha kuku hutumiwa kama mbolea ya kikaboni baada ya kuoza. Vifaranga hupenda kula mchanga na mkaa kwa usagaji wa chakula kwa urahisi. Epuka kuzaliana kati ya kuku walio katika familia hiyo hiyo, kwani huku kunaweza kusababisha kuku dhaifu. Weka vijiti kimlalo juu ya sakafu ili ndege waweze kupumzikia usiku na kukusanya kinyesi kwa urahisi.

Hatua za utunzaji

Jenga banda la kuku ili kuwalinda dhidi ya ndege wawindaji, wezi na hali mbaya ya hewa. Safisha banda mara kwa mara ili kuku waweze kuwa na afya bora. Nyunyiza majivu sakafuni ili kupunguza kushambuliwa na vimelea vidogo kama utitiri na kupe. Weka pumba za mbao au nyasi kavu ili kuandaa eneo la kutaga mayai, na pia kupunguza kushambuliwa na vimelea.

Udhibiti wa vimelea

Kuku anapotaga mara mbili, nyunyizia masanduku ya kutagia kwa acaricide, na majivu ili kudhibiti vimelea. Daima, funga ndege wadogo wakati wa wiki za kwanza ili kuwalinda dhidi ya wanyama waharibifu na kupotea. Wotolee vifaranga joto katika siku za baridi ili kudhibiti kifo. Unaweza hata kuwapa mchanganyiko wa ngano, shayiri, mahindi na majani kwa kuwa ni nafuu. Safisha vyombo vya maji kila mara na wape maji safi ili kuepuka magonjwa. Ongeza dawa za kienyeji kama vile majani ya mshubiri, pilipili kwenye maji ya kunywa ili kuimarisha kinga ya kuku dhidi ya magonjwa. Wazike ndege waliokufa ili kuepuka kuambukiza kuku wenye afya.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:55Kuku ni chanzo cha protini na mapato kwa wafugaji.
00:5601:04Hatua za kukuza kuku wenye afya bora.
01:0501:36Epuka kuzaliana kati ya ndege wa familia hiyo hiyo
01:3702:13Andaa banda la kuku huku ukiweka vijiti kimlalo juu ya sakafu
02:1403:16Safisha makazi mara kwa mara na unyunyizie majivu chini.
03:1704:35Tayarisha kitanda cha pumba za mbao au nyasi kavu.
03:3605:29Kuku anapotaga mara ya pili, nyunyizia dawa kwenye masanduku.
05:3005:49Funga ndege wachanga katika banda wakati wa wiki za kwanza na, wape joto katika siku za baridi.
05:5006:09Wape ndege mchanganyiko wa ngano, shayiri, mahindi na majani.
06:1006:25Safisha vyombo vya maji safi na wape kuku maji safi kila siku.
06:2607:19Chanja kuku dhidi ya magonjwa, na dhibiti wadudu. Kideri huua kuku kwa urahisi.
07:2008:20Ongeza dawa za kienyeji kwa maji ya kunywa.
08:2108:31Zika ndege waliokufa walioambukizwa.
08:3209:40Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *