»Usimamizi wa bakajani ya bakteria kwenye mpunga«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/managing-bacterial-leaf-blight-rice

Muda: 

00:13:00
Imetengenezwa ndani: 
2018

Imetayarishwa na: 

MSSRF

Bakajani ( bacterial leaf blight) inaweza kuharibu hadi nusu ya mavuno yako. Kwa hivyo ni muhimu kujua jinsi ya kuzuia ugonjwa huo.

Bakajani huonekana sana katika mwanzo wa msimu, na husambaa hasa kupitia kwenye mbegu, vidonda, maji ya mvua na maji ya umwagiliaji. Unapopanda aina majo kila mwaka, ugonjwa huo unaweza kuwa na mlipuko mkubwa. Bakajani hupatikana pia kwenye magugu, na mapaki ya mazao na inaweza kushambulia mavuno yako kuto kwenye hayo.

Bakajani ya bakteria

Ugonjwa huu huathiri mimea ya mpunga katika kitalu na zao kuu la shamba. Unaweza kuitambua, kwa sababu ncha ya majani ya mpunga hukauka. Kisha bakajani huenea chini ya upindo wa majani. Bakajani huonekana kama hali ya muundo wa wimbi. Mwishowe hukausha mmea wako.

Unapotaka kuangalia ikiwa mimea yako ina ugonjwa, unaweza kukata majani yalio na ugonjwa na kuiweka kwenye kikombe kilichojazwa na maji. Ikiwa majani hutoa majimaji ya hudhurungi ambayo hutokana na bakteria, unajua kuwa mimea yako imeathiriwa. Hii haimaanishi kwamba mimea yako yote itaugua, bali ugonjwa unaweza kuharibu karibu nusu ya shamba. Kutoka umbali kadha, unaweza kuona vizuri ni mimea mingapi imeathiriwa.

Usimamizi wa ugonjwa

Ili kudhibiti ugonjwa, panda mbegu zilizo na afya, na sugu dhidi ya ugonjwa wa bakajani. Unafaa daima kuondoa magugu na mabaki ya mazao shambani lako na uyaoze.

Baadaye katika msimu,usikate majani yaliyoathiriwa, kwa sababu hapo ugonjwa unaweza kuenea kwa urahisi. Virutubisho kama zinc na copper husaidia kujenga mmea na kuufanya uwe sugu zaidi.

Mara tu unapogundua majani makavu, unafaa kuchanganya kilo 40 za samadi mbici ya ng‘ombe na lita 100 za maji kwa nusu hekta. Acha ikae kwa masaa 24. Kisha koroga samadi na uchuje kwa mfuku. Baadaye unaweza kuongeza lita 100 za maji. Nyunyizia mchanganyiko huo kwa siku 15, kila siku mara tatu.

Unaweza pia kutumia kilo 1 ya Pesudomonas-talc kutoka dukani, na lita 200 za maji kwa nusu hekta. Tumia mchanganyiko huu siku 15 baada ya kupandikiza. Siku 10 baadaye, nyunyiza tena, na kisha baada ya siku 10 nyingine ongeza kunyunyiza mchanganyiko huo.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:30Utangulizi
00:3101:35Bakajani inaweza kuharibu hadi nusu ya mavuno yako.
01:3602:53Ncha ya majani ya mpunga hukauka. Kisha bakajani huenea chini ya upindo wa majani, na mwishowe kukausha mmea wako
02:5403:08Majani yalio athiriwa na ugonjwa hutoa majimaji yakikatwa na kuyaweka kwenye kikombe kilichojazwa na maji.
03:0903:28Bakajani husambaa hasa kupitia kwenye mbegu, vidonda, maji ya mvua na maji ya umwagiliaji. Bakajani hupatikana pia kwenye magugu, na mapaki ya mazao
03:2905:45Panda mbegu zilizo na afya, na sugu dhidi ya ugonjwa wa bakajani.
05:4606:30Keep the field free from weeds. Daima ondoa magugu shambani mwako.
06:3106:55Virutubisho kama zinc na copper husaidia kujenga mmea na kuufanya uwe sugu zaidi.
06:5607:36Usikate majani yaliyoathiriwa, kwa sababu hapo ugonjwa unaweza kuenea kwa urahisi.
07:3708:50Changanya samadi mbici ya ng‘ombe maji.
08:5109:36Unaweza pia kutumia Pesudomonas-talc
09:3709:50Unafaa daima kuondoa magugu na mabaki ya mazao Shambani lako na uyaoze.
09:5110:53Unapopanda aina majo kila mwaka, ugonjwa huo unaweza kuwa na mlipuko mkubwa
10:5412:47muhtasari
12:4813:00Mikopo

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *