»Ugonjwa wa Matekenya/ Michirizi ya Kahawia (CBSD) katika mihogo«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=O__LVsNZmRw

Muda: 

00:19:51
Imetengenezwa ndani: 
2012

Imetayarishwa na: 

AIRC National Documentarie

Uzalishaji wa muhogo huathiriwa zaidi na magonjwa mawili; ugonjwa wa batobato(CMD), na matekenya (CBSD). Matekenya huathiri mmea mzima na naweza kusababisha hasara kubwa sana.

Ugonjwa matekenya huenezwa na wadudu kwa mfano nzi weupe. Visu vinavyotumika kukata mashina ya muhogo ulioathirika pia hueneza ugonjwa huo vikitumika kukata shina la muhogo wenye afya, na wakati shina la mmea ulioathirika linapogusana na shina la mmea wenye afya hasa wakati wa upepo.

Dalili za ugonjwa wa matekenya

Dalili za ugonjwa wa matekenya huonekana kwenye majani, mashina na mizizi.

Majani hugeuka manjano, michirizi ya kahawia/michibuko kwenye shina, na katika hali mbaya mmea hukauka kutoka kwenye ncha kwenda chini. Dalili muhimu zaidi ni zile zinazoonekana kwenye mizizi. Umbo la mzizi hupinda na sehemu ya ndani ya mzizi inayoweza kuliwa huonekana kahawia, huoza na huwa ngumu.

Ugonjwa huo huenezwa kwa kutumia vipandikizi vilivyoambukizwa na kupitia eneo la kuzidishia mbegu, iwapo chanzo asili kiliambukizwa.

Udhibiti wa matekenya

Kwa kuanzia, usimamizi ni kuhakikisha unapanda vipandikizi vya mihogo isiyo na magonjwa. Epuka kugawana vifaa vya shambani kwani haku kunaweza kusababisha maambukizi ya ugonjwa huo kutoka shamba moja hadi jingine. Panda aina za mihogo inayostahimili magonjwa. Mimea iliyoambukizwa inapaswa kung‘olewa na kuharibiwa kwa kuwa ni chanzo cha viini vinavyosababisha ugonjwa huo.

Wakati wa kuzidisha vipandikizi vya muhogo, ukaguzi wa shamba kwa ugonjwa wa matekenya ufanyike na wafanyakazi wenye ujuzi.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0003:10Ugonjwa wa matekenya unaweza kusababisha hasara ya hadi 100% katika mavuno ya muhogo.
03:1105:11Ugonjwa wa matekenya huenezwa na wadudu kwa mfano nzi weupe.
05:1205:34Visu vinavyotumika kukata mashina ya muhogo pia hueneza virusi na wakati shina la mmea wenye ugonjwa unaposugua mmea wenye afya.
05:3509:18Dalili za CBSD ni pamoja na; majani hubadilika manjano, michibuko au vidonda kwenye shina, mmea hukauka kutoka kwenye ncha kwenda chini
09:1910:36Dalili muhimu zaidi ni zile zinazoonekana kwenye mizizi. Umbo la mizizi hupinda na sehemu ya ndani huwa kahawia, huoza na hubadilika ngumu.
10:3711:47Ugonjwa huu huenezwa kwa kutumia mimea iliyoambukizwa na kwa kuzidisha aina mbalimbali.
11:4813:27Usimamizi ni kwa kupanda vipandikizi visivyo na magonjwa, epuka kugawana zana za bustani kati ya mashamba, kuharibu mimea iliyoambukizwa na kupanda aina sugu
13:2815:29Wakati wa kuzidisha nyenzo za kupanda muhogo, kagua shamba kwa uwepo wa ugonjwa, na tumia wafanyakazi wenye ujuzi.
15:3018:44Ugonjwa wa matekenya (michirizi ya kahawia wa mihogo) una dalili tofauti na ugonjwa wa batobato
18:4519:51Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *