»Udhibiti wa ugonjwa wa kiwele«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=3zit1UNp7iM&t=23s

Muda: 

00:08:27
Imetengenezwa ndani: 
2016

Imetayarishwa na: 

Digital Agriculture

Ugonjwa wa kiwele ni vimbe wa kiwele cha mnyama unaodhihirishwa na mabadiliko ya kiwele na maziwa kimwili, kikemikali na kibaolojia.

Ugonjwa huu husababishwa na bakteria kupitia mazingira ya ukamuaji yasio safi. Hata hivyo, unaweza kudhibitiwa kwa kufuata kanuni za usafi za ukamuaji. Kwa hivyo ni muhimu kutambua na kudhibiti ugonjwa huo ili kupunguza hasara ya kiuchumi. Ni muhimu kusafisha kiwele kilichoathiriwa kabla ya uchunguzi. Tumia kikombe cha kupima ugonjwa.

Dalili

Kuna dalili nyingi za ugonjwa wa kiweleambazo ni pamoja na, uvimbe wa kiwele, mabadiliko ya rangi ya maziwa, maziwa huganda, uwepo wa damu kwenye maziwa, uwepo wa usaha, ugumu wa kiwele, kupunguka kwa kiwango cha maziwa, homa, na ulaji mdogo wa chakula.

Matibabu

Kamua maziwa yote kutoka kwa kiwele kilichoathiriwa baada ya uthibitisho wa kuwepo kwa ugonjwa ili kuimarisha matibabu zaidi.

Weka viuavijasumu ndani ya matiti yaliyoathiriwa kwa matibabu bora.

Hatua za udhibiti

Kamua wanyama walioambukizwa mwisho ili kudhibiti kuenea kwa magonjwa kwa wanyama ambao hawajaambukizwa.

Vile vile osha mikono vizuri kabla na baada ya kukamua. Usiruhusu mnyama kulala chini baada ya kukamua ili kuepuka maambukizi kwa matiti.

Hatimaye kusanya maziwa ya kwanza ya kila titi kivyake ili kuwezesha upimaji sahihi wa ugonjwa.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:42Ugonjwa wa kiwele ni vimbe wa kiwele unaodhihirishwa na mabadiliko ya kiwele cha mnyama.
00:4301:06Ni muhimu kutambua na kudhibiti ugonjwa huo
01:0701:52Safisha kiwele kilichoathiriwa kabla ya uchunguzi. Tumia kikombe cha kupima ugonjwa.
01:5302:30Dalili za ugonjwa ni pamoja na, uvimbe wa kiwele, mabadiliko ya rangi ya maziwa, maziwa huganda, uwepo wa damu kwenye maziwa, uwepo wa usaha.
02:3103:12Kamua maziwa yote kutoka kwa kiwele kilichoathiriwa baada ya uthibitisho wa kuwepo kwa ugonjwa
03:1304:41Weka viuavijasumu ndani ya matiti yaliyoathiriwa
04:4205:35Wape wanyama viuavijasumu.
05:3606:09Udhibit; Kamua wanyama walioambukizwa mwisho,osha mikono vizuri kabla na baada ya kukamua.
06:1006:50Usiruhusu mnyama kulala chini baada ya kukamua. kusanya maziwa ya kwanza ya kila titi kivyake.
06:5107:20Dalili kuu ni pamoja na ; ugumu wa kiwele, kiwele kuvimba na maumivu.
07:2107:33Kupunguka kwa kiwango cha maziwa, homa, na ulaji mdogo wa chakula.
07:3408:00Ugonjwa huu husababishwa na bakteria kupitia mazingira ya ukamuaji yasio safi.
08:0108:27Ugonjwa huo unaweza kudhibitiwa kwa kufuata kanuni za usafi za ukamuaji.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *