»Kulisha Konokono«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/feeding-snails

Muda: 

00:09:24
Imetengenezwa ndani: 
2016

Imetayarishwa na: 

AMEDD, MOBIOM, Songhaï Centre

Konokono huishi katika mazingira yenye unyevu mwingi, na hukusanywa kijadi ili kuliwa. Nyama yao ni nzuri kwani imekithiri protini, madini na kalisiam kuliko nyama ya ng‘ombe hata na maini. Ni muhimu sana kwa watoto, na wanawake wajawazito au wanaonyonyesha.

Kuongezeka kwa idadi ya watu, uharibifu wa misitu na upanuzi wa kilimo hufanya ukusanyaji wao mwituni kuwa mgumu. Kwa hivyo, kuna hitaji la kilimo cha konokono. Kusimamia shamba la konokono ni rahisi kwani halihitaji rasilimali nyingi, nafasi kubwa au wakati. Kwa hivyo, kilimo hiki kinaweza kuongeza mapato kwa mkulima.

Konokono hula nyenzo za mimea kama vile majani, matunda na mizizi. Malisho ya ziada husaidia konokono kufikia 400-500 g kwa miezi 4.

Kuandaa chakula cha konokono

Vipimo 3 vya wishwa ya ngano vinachanganywa na vipimo 3 vya keki ya nazi, vipimo 3 vya makombe yaliyosagwa na kipimo 1 cha keki ya soya. Ngano hutoa nguvu, keki ya nazi hutoa nguvu na protini, makombe ya chaza hutoa kalsiamu, na keki ya soya hutoa protini.

Iwapo hakuna rasilimali ya kutosha, unaweza kuandaa lishe ukutumia wishwa ya mahindi au mchele. Keki ya njugu au unga wa samaki unaweza kutumika kama chanzo cha protini. Kalsiamu husaidia kuimarisha makombe. kombe la yai, kombe la konokono au mifupa ya wanyama inaweza kusagwa baada ya kuchomwa motoni, na kuchanganywa na lishe. Konokono hula udongo pia ambao una virutubisho na kalsiamu

Kulisha konokono

Konokono hulishwa mara moja kwa siku wakati wa jioni kwa sababu hutoka usiku tu. Wape konokoko maji ukitumia chombo kilicho na kina kifupi ili kuruhusu konokono kunywa vizuri. Eneo la kulisha linafaa pia kuwa safi.

Tahadhari: Usiwape konokono Malishe machungu kama vile mwarobaini, papai na majani ya mtukutu kwani huathiri ladha. Kuwalisha konokono lishe tamu husababisha ladha nzuri.

Kamwe, usichanganye chumvi kwenye lishe kwani chumvi hukausha maji mwilini na kuua konokono.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:27Konokono huishi katika mazingira yenye unyevu mwingi, na hukusanywa kijadi ili kuliwa.
00:2800:40Konokono hutoa mapato. Nyama yao ni nzuri kwani imejaa protini, madini na kalisiam, na ni muhimu sana kwa watoto, na wanawake wajawazito au wanaonyonyesha.
00:4101:11Ukusanyaji wao mwituni umekuwa mgumu. Kwa hivyo, kuna hitaji la kilimo cha konokono
01:1201:48Kusimamia shamba la konokono ni rahisi kwani halihitaji rasilimali nyingi, nafasi kubwa au wakati.
01:4902:18Konokono hula nyenzo za mimea kama vile majani, matunda na mizizi
02:1905:33Konokono hulishwa mara moja kwa siku wakati wa jioni
05:3405:59Wape konokoko maji ukitumia chombo kilicho na kina kifupi ili kuruhusu konokono kunywa vizuri.
05:6006:02Eneo la kulisha linafaa pia kuwa safi kabla ya kuweka chakula.
06:0306:16Chakula kinafaa kuwekwa mahali pasipo na ncha zilizoinuliwa.
06:1706:30Konokono hukua haraka wakipewa milisho ya mchanganyiko
06:3106:48Usiwape konokono Malishe machungu kwani huathiri ladha
06:4907:41Kamwe, usichanganye chumvi kwenye lishe kwani chumvi hukausha maji mwilini na kuua konokono.
07:4109:24Muhtasari.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *