»Kukuza tikitimaji. Jinsi ya kupanda, kukuza na kuvuna matikitimaji«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=apgo4I_RP0U&list=RDCMUCOL8wsKTTsgkAiLGzcT-Gdg&index=37

Muda: 

00:06:15
Imetengenezwa ndani: 
2014

Imetayarishwa na: 

infoagrocom

Kwa kuwa ni tunda lenye virutubisho vingi, ubora na wingi wa tikitimaji hutegemea teknolojia na mbinu za kilimo zinazotumiwa na mkulima.

Kwa kuwa ni mmea wa majani, ambao hudumu kwa mwaka, tikitimaji ni jamii ya cucurbitaceae na jina lake la kisayansi ni citrullus lanatus. Mchakato wa kupanda mmea huanza kwa kupanda mbegu kwenye vitalu, na mmea unapokua hadi urefu wa 8cm, majani makuu huanza kuonekana.

Usimamizi wa tikiti maji

Siku 10–12 baada ya kuota, jani la kwanza hukauka na kijicho huanza kuchipuka. Ili kuzuia magonjwa katika vitalu vya plastiki, bebesha au unganisha miche kwa kutumia mabua ya malenge kama njia ya kuongeza upinzani dhidi ya mnyauko wa fusari na magonjwa mengine ya ukungu yanayopatikana kwenye udongo. Muda kati ya kupanda na kupandikiza hutofautiana kutoka siku 30–40 tangu wakati wa kupanda mbegu kwenye kitalu.

Pandikiza miche kwenye udongo bila kutenganisha mizizi. Funika mzizi kwa udongo na umwagilie maji ili kustawisha mmea. Mwezi mmoja baada ya kupanda, mtikitimaji huanza kuchipuka matawi yanayotambaa na majani huanza kugawanyika.

Mwagilia mimea siku 10–12 baada ya umwagiliaji wa kwanza. Baada ya mtikitimaji kutoa majani mengi, tengeneza mitaro au matuta. Kupogoa kwa kwanza hufanywa wakati majani 4–6 halisi yanapotokea.

Vile vile, mchakato huo hurudiwa wakati matawi ya pili yanapotokea. Katika kupogoa kwa pili, ni matawi mawili tu kuu yanayoachwa. Wakati matawi haya yana majani 5–6, vijicho huodolewa ili kuruhusu uundaji wa matawi ya pili.

Funika udongo na damani ya plastiki, mboji au mchanga ili kudumisha joto la udongo na unyevu wa udongo. Wakati wa kuchanua maua, maua ya kwanza kuonekana ni ya kiume yakifuatiwa na yale ya kike ambayo hukua kutoka kwenye tawi kuu na machipukizi ya pili.

Kwa uchavushaji, vichocheo bandia huwekwa kwenye chafu ili kusababisha ukuaji wa matunda. Aina amabyo hukomaa mapema huanza kuzaa matunda kwa mwezi 1.5 na kwa miezi 2, mabua yatakuwa na urefu wa mita 1. Kutoka wakati huu mmea huwa unahitaji joto la muda mrefu.

Hatimaye, siku ya kuvunia hutegemea aina iliyopandwa, eneo, wakati wa kupandia na mfumo wa kilimo uliotekelezwa. Wakati mzuri wa kuvunia ni asubuhi.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:24Tikitimaji ni mmea wa majani, ambao hudumu kwa mwaka, na ni jamii ya cucurbitaceae
00:2501:00Mchakato wa kupanda mmea huanza kwa kupanda mbegu kwenye vitalu
01:0101:13Mmea unapokua hadi urefu wa 8cm, majani makuu huanza kuonekana.
01:1401:22Siku 10–12 baada ya kuota, jani la kwanza hukauka
01:2301:48Ili kuzuia magonjwa katika vitalu vya plastiki, bebesha au unganisha miche kwa kutumia mabua ya malenge.
01:4901:56Muda kati ya kupanda na kupandikiza hutofautiana kutoka siku 30 hadi 40
01:5702:19Pandikiza miche kwenye udongo na mwagilia maji.
02:2002:26Mwezi mmoja baada ya kupanda, mtikitimaji huanza kuchipuka matawi yanayotambaa na majani huanza kugawanyika.
02:2702:34Mwagilia mimea siku 10–12 baada ya umwagiliaji wa kwanza.
02:3502:48Baada ya mtikitimaji kutoa majani mengi, tengeneza mitaro au matuta
02:4903:10Kupogoa kwa kwanza hufanywa wakati majani 4–6 halisi yanapotokea.
03:1103:23Mchakato huo hurudiwa wakati na matawi ya pili yanapotokea
03:2403:27Katika kupogoa kwa pili, ni matawi mawili tu kuu yanayoachwa
03:2803:40Wakati matawi haya yana majani 5–6, vijicho huodolewa
03:4104:01Funika udongo na damani ya plastiki, mboji au mchanga
04:0204:14Maua ya kwanza kuonekana ni ya kiume yakifuatiwa na yale ya kike
04:1404:23Maua ya kike hukua kutoka kwenye tawi kuu na machipukizi ya pili.
04:2404:56Kwa uchavushaji, vichocheo bandia huwekwa kwenye chafu
04:5705:04Aina amabyo hukomaa mapema huanza kuzaa matunda kati ya mwezi 1.5-2.
05:0405:17Kutoka wakati huu mmea huwa unahitaji joto la muda mrefu.
05:1805:25Siku ya kuvunia hutegemea aina iliyopandwa, eneo, wakati wa kupandia na mfumo wa kilimo uliotekelezwa
05:2605:40Kipindi cha miezi 2–3 kinapita kutoka kwa kupanda hadi kuanza kuvuna.
05:4105:55Wakati mzuri wa kuvunia ni asubuhi.
05:5606:11Tikit maji ni tunda kubwa lenye nyama laini , rangi umbo tofauti.
06:1206:15Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *