»Kudhibiti matekenya (mealybugs) katika mihogo«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/managing-mealybugs-cassava

Muda: 

00:16:00
Imetengenezwa ndani: 
2016

Imetayarishwa na: 

Agro-Insight

Ulimwenguni kwote, mihogo hukuzwa kwa wanga na mizizi yake inayoliwa, lakini huathiriwa na wadudu na magonjwa. Matekenya ni moja wapo ya wadudu wakubwa ambao hushambulia mihogo, na wanahitaji kudhibitiwa.

Kuna aina nyingi ya matekenya, wote wakiwa na maumbo tofauti. Wanaweza kuwa weupe, wekundu au kijani. Wote wanaweza kudhibitiwa kwa njia sawa. Matekenya wanaweza kuenezwa kupitia upepo, maji na wanadamu. Mimea ya mihogo iliyoshambuliwa hutoa mizizi midogo.

Kudhibiti matekenya

Matekenya wanaweza kudhibitiwa na kuzuiwa kwa mbinu kadhaa ambazo ni pamoja na kuondoa na kuchoma mabaki ya mimea iliyoathiriwa baada ya kuvuna. Hii huzuia upitishaji wa matekenya kwa msimu ujao. Kupanda mazao mengine kama vile mahindi, miwa au mazao yoyote yasiyopokea matekenya. Unaweza tena kupanda mihogo baada ya mazao mengine kuvunwa. Panda mapema katika mwanzo wa mvua, kwani maji hudondosha matekenya. Kwa hivyo, kunasalia matekenya wachache kwa mimea, au wote huondolewa.

Awali, panda mbegu zenye afya na zilizowekwa kwenye dawa ili kuua viini. Hatua hizi hufanywa ili kuwezesha kupanda mbegu ambazo hazina matekenya. Kukagua shamba mara kwa mara katika msimu wote ili kuondoa ncha zilizoathiriwa na matekenya hupunguza magonjwa kuenea. Mabaki ya mimea na vipande vilivyoondolewa huchomwa ili kuua matekenya.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0002:13Matekenya ni moja wapo ya wadudu wakubwa ambao hushambulia mihogo, na wanahitaji kudhibitiwa.
02:1402:53Kuna aina nyingi ya matekenya, wote wakiwa na maumbo tofauti. Wanaweza kuwa weupe, wekundu au kijani
02:5403:48Tekenya mmoja anaweza kuzaa wengine wengi, na hivyo kushambulia muhogo kwa haraka sana. Matekenya hutaga mayai yao kwenye kifuko cheupe kinachokaa kama pamba kwenye mmea wa muhogo.
03:4904:40Mihogo iliyoathiriwa na matekenya hutoa mizizi midogo. Matekenya hudondosha maji maji matamu ambayo huvutia chungu. Uwepo wa chungu unaweza kuwa ishara ya shambulio la matekenya.
04:4105:16Matekenya wanaweza kuenezwa kupitia upepo, maji na wanadamu.
05:1707:15Ili kudhibiti matekenya, ondoa na kuchoma mabaki ya mazao yaliyoambukizwa.
07:1607:34Fanya mzunguko wa mazao kwa kupanda mahindi, miwa au zao lingine lolote.
07:3507:53Panda mihogo mwanzoni mwa msimu wa mvua.
07:5408:26Nunua na kupanda mbegu za muhogo ambazo hazijaambukizwa.
08:2709:12Tumia mbolea kukuza mimea yenye nguvu.
09:1310:19Kuua viini viliyo kwenye mbegu za muhogo
10:2011:55Kutumia maadui asili wa matekenya
11:5612:44Tutumia dawa za kuua wadudu, lakini hizi ni ghali.
12:4512:57Kukagua shamba mara kwa mara katika msimu wote ili kuondoa ncha zilizoathiriwa na kuzichoma.
12:5813:30Jitihada za pamoja kudhibiti matekenya.
13:3116:00Muhtasari.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *