»Kudhibiti chule (anthracnose) katika maembe«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/managing-anthracnose-mango

Muda: 

00:17:06
Imetengenezwa ndani: 
2017

Imetayarishwa na: 

Christoph Arndt, Holger Kahl, JFP films

Chule ni ugonjwa hatari wa kuvu ambao huathiri maembe. Chule hustawi vizuri katika hali ya mvua na unyevu. Ugonjwa huu unaweza kudhibitiwa kwa kupogoa, na kutumia viuakuvu.

Ugonjwa huu husababisha uharibifu mkubwa shambani, lakini pia huharibu matunda baada ya kuvuna, na hivyo ni changamoto kubwa kwa soko la kuuza nje.

Chule hutambuliwa na uwepo wa madoa meusi kwenye majani ambao huwa madogo awali, na baadaye hupanuka. Chule husababisha mashimo kwenye majani, ambayo hukauka mwishowe. Ugonjwa huo huenezwa kupitia kwa mvua, na maambukizo huanzia kwa majani, huenea kwa matawi, na kisha kwa maua na mwishowe mmea wote.

Hatua za udhibiti

Kagua shamba lako mara kwa mara na ufuatilie mabadiliko ya hali ya hewa kwa sababu chule hudhuru sana baada ya mvua.

Ondoa sehemu zilizoambukizwa, haswa maembe madogo na yaliyooza. Hizi hufanya kama chanzo cha kueneza ugonjwa.

Pogoa matawi ya mti ili kuwezesha upenyezaji wa mwanga wa jua. Hii huzuia hali ya unyevu ambayo husababisha chule.

Matumizi ya dawa ya viuakuvu

Kuyunyiza viuakuvu tu haitoshi, bali ni bora kuvitumia pamoja na udhibiti wa mikono. Viuakuvu vinaweza kuwa vya mugusano (viuakuvu vya shaba) au vya kimfumo. Tumia viuakuvu vya shaba wakati dalili za ugonjwa za kwanza zinapoonekana, na viuakuvu vya kimfumo muda mfupi kabla ya maua kutoka. Walakin, usitumie viuakuvu wakati wa maua kuchana, kwasababu huwa vitaharibu maua. Endelea kunyunyizia dawa kila baada ya wiki 3 hadi 4, huku ukibadilisha kati ya viuakuvu vya kimfumo na vya msugano.

Sitisha kunyunyizia viuakuvu hivyo wiki 3 kabla ya kuvuna, lakini waweza kutumia vile vilivyo na viambato tofauti.

Changanya rangi ya chakula na maji, na umwagiliae mchanganyiko huo kwenye mti kutoka juu hadi chini. Tahadhari kuangalia ni kiasi gani kinachotumika. Panua kiwango hiki ukitegemea idadi ya miti uliyonayo ili kukadiria kiwango cha kemikali kinachohitajika.

 

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0001:31Chule ni changamoto kubwa katika kilimo cha embe haswa katika maeneo ya hali ya hewa ya unyevu.
01:3202:53Chule hutambuliwa na uwepo wa madoa meusi kwenye majani ambao huwa madogo awali, na baadaye hupanuka.
02:5403:22Chule ni ugonjwa hatari wa kuvu ambao huathiri maembe na hustawi vizuri katika hali ya mvua na unyevu. Sehemu za mmea zilizoambukizwa ni chanzo cha magonjwa na huenezwa na mvua.
03:2304:27Chule ni changamoto kubwa kwa matunda ya soko la kuuzia nje. Husababisha uharibifu shambani na baada ya mavuno.
04:2805:23Kagua shamba lako mara kwa mara. Chule hudhuru sana baada ya mvua
05:2407:49Ondoa sehemu za mmea zilizoambukizwa, Pogoa matawi ya mti.
07:5008:59Kuyunyiza viuakuvu pamoja na udhibiti wa mikono. Viuakuvu vinaweza kuwa vya mugusano (viuakuvu vya shaba) au vya kimfumo
09:0009:39Tumia viuakuvu vya shaba wakati dalili za ugonjwa za kwanza zinapoonekana, na viuakuvu vya kimfumo muda mfupi kabla ya maua kutoka. Walakin, usitumie viuakuvu wakati wa maua kuchana.
09:4010:02Endelea kunyunyizia dawa kila baada ya wiki 3 hadi 4, huku ukibadilisha kati ya viuakuvu vya kimfumo na vya msugano.
10:0310:50Sitisha kunyunyizia viuakuvu hivyo wiki 3 kabla ya kuvuna
10:5112:50Changanya rangi ya chakula na maji, na umwagiliae mchanganyiko huo kwenye mti kutoka juu hadi chini
12:5115:28Nyunyizia kila mti kwa usahihi, lakini epuka kumwagilia wakati mvua inatarajiwa kunyesha katika siku 3 zijazo.
15:2917:06Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *