»Kilimo cha malisho ya ng‘ombe wa maziwa kwa ufanisi nchini Kenya – Sehemu ya 3«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=e5UraqlaH64

Muda: 

00:09:25
Imetengenezwa ndani: 
2022

Imetayarishwa na: 

Farm Kenya

Kunyausha ni mchakato wa kuacha mmea shambani baada ya kukatwa ili uweze kukauka. Kisha mmea hukusanywa na hutumika kama malisho ya mifugo.

Baada ya kuvuna mimea, itandaze kwenye jua kwa masaa machache ili inyauke. Katakata na kuchanganya mimea iliyonyauka na malisho mengine kama vile mabua ya mahindi au nyasi ya napier, na kisha ulishe mifugo. Kwa siku, ng‘ombe anaweza kulisha hadi kilo 70 za malisho ambayo hayajakaushwa, na kilo 20 tu kwa malisho yaliyokaushwa. Kulisha mifugo malisho yenye unyevu husababisha uyabisi wa tumbo hasa kwa ndama. Mihogo pia inaweza kutumika kama malisho ya mifugo, kwani majani yake yana vitamini na protini kwa kiasi cha 16% –18%.

Kutumia mihogo

Unapotengeneza silaji unaweza kuchagua kuchanganya majani ya muhogo na silaji ya napier au silaji ya mahindi ili kuongeza viwango vya protini. Mbegu za muhogo hazitumiki.

Malisho ya muhogo ni bora kwa mbuzi wa maziwa kwani ni mbadala wa protini.

Malisho mengine zaidi

Calliandra calothyrsus inayojulikana kama mti wa calliandra ni kichaka cha malishe ambacho kinaweza kukuzwa, na hakina miiba. Pia kinaweza kutumika kama mbadala wa malisho ya kutoa maziwa. Ni rahisi kukuza na kutunza, hukua haraka, hustahimili udongo wenye tindikali, na husaidia kuongeza nitrojeni kwenye udongo.

Unapolisha wanyama, mtolee kila mnyama 2kg-4kg kwa siku. Thamani ya lishe ya mti hupungua kadri unavyochanua maua.

Faida za calliandra

Calliandra hutolea mbuzi protini nzuri, nishati na madini. Huongeza uzalishaji wa maziwa kwa mbuzi kutoka lita 1 –2 lita kwa siku. Calliandra huboresha rutuba ya udongo, na husaidia kudhibiti mmomonyoko wa udongo katika maeneo wazi.

Pia ni hutoa kuni kwani hukua haraka, na hutoa mkaa. Majani yanaweza kutumika kama matandazo shambani, na kama mbolea ya kijani kwani huongeza nitrojeni kwenye udongo.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0001:30Kunyausha ni mchakato wa kuacha mmea shambani baada ya kukatwa ili uweze kukauka.
01:3102:41Kuchanganya desmodium na malisho kama vile mabua ya mahindi au nyasi ya napier.
02:4203:46Kiasi cha kulisha mnayama kwenye lishe kavu na lishe mbichi.
03:4704:41Mihogo pia inaweza kutumika kama malisho ya mifugo, kwani majani yake yana vitamini na protini kwa kiasi cha 16% –18%.
04:4205:20Kutumia majani ya muhogo kama malisho.
05:2106:09Mti wa Calliandra kama malisho na sifa zake.
06:1007:26mti wa callandra.
07:02708:23Faida za mti wa callindra.
08:2409:25Umuhimu wa Calliandra.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *