»kilimo cha mahindi sehemu ya pili«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=XxjsvQNNn08

Muda: 

00:08:35
Imetengenezwa ndani: 
2018

Imetayarishwa na: 

royaldreamtv

Mahindi yamekithiri wanga, protini na madini, na hutumiwa kama msingi wa wanga katika milo mbalimbali duniani kote.

Kuna wadudu na magonjwa kadhaa ambayo husababisha upungufu wa mavuno ya mahindi. Magonjwa ni pamoj na ukungu, ubwiri unga, madoa, kuoza kwa mizizi, bakajani, chule na wadudu waharibifu ni panzi, viwavi jeshi, mchwa nakadhalika. Magonjwa hayo husababishwa na bakteria, fangasi na virusi na yanaweza kudhibitiwa kwa kusafisha mashamba baada ya kuvuna, kubadilisha mazao, kupanda aina sugu na kudhibiti wadudu. Ili kudhibiti wadudu, nyunyiza na kemikali zinazopendekezwa, haribu vilima vya mchwa shambani.

Mbinu za kilimo

Unapopanda, weka kilo 200 za NPK kwa hekta kwa udongo wenye rutuba, na kilo 600 kwa udongo usio na rutuba. Mbolea huongezwa katika hatua mbili ambazo ni wakati wa kupanda na wiki 5 hadi 6 baadaye. Dhibiti magugu ili kupunguza ushindani wa virutubisho, na pia dhibiti wadudu na magonjwa.

Runda udongo kuzunguka mmea ili kufunika mizizi iliyo wazi. Palilia wiki 2 baada ya kupanda na weka mbolea kabla ya kupalilia mara ya pili yaani baada ya wiki 6 hadi 7.

Dhibiti wadudu na magonjwa kwa kuchagua aina sugu, na kutumia kemikali inayopendekezwa. Iwapo mkulima hana pesa, nyunyiza mimea kwa mchanganyiko wa maji na sabuni ambao hudhibiti viwavijeshi.

Baada ya kuvuna, changanya mabua ya mimea kwenye udongo ili kuongeza mboji na kuboresha rutuba na uzalishaji.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:40Unapopanda, weka kilo 200 za NPK kwa hekta kwa udongo wenye rutuba, na kilo 600 kwa udongo usio na rutuba
00:4102:13Dhibiti magugu runda udongo kuzunguka mmea
02:1402:48Palilia wiki 2 baada ya kupanda na weka mbolea kabla ya kupalilia mara ya pili yaani baada ya wiki 6 hadi 7.
02:4905:02Dhibiti wadudu na magonjwa kwa kuchagua aina sugu, na kutumia kemikali inayopendekezwa
05:0305:23Nyunyiza mazao na maji yaliyochanganya na sabuni.
05:2406:06Kwa magonjwa nyunyiza na kemikali.
06:0706:34Baada ya kuvuna, changanya mabua ya mimea kwenye udongo
06:3506:52Magonjwa ya mahindi husababishwa na; bakteria, fungi na virusi.
06:5307:03Magonjwa husababisha mimea kudumaa, kunyauka na kufa.
07:0407:18Safisha shamba, zungusha mazao, panda aina sugu na dhibiti magonjwa na wadudu.
07:1907:48Mahali ambapo wadudu hugunduliwa nyunyiza dawa mara moja.
07:4908:14Haribu vilima vya mchwa ndani na karibu na shamba.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *