»Jinsi ya kupogoa – Usimamizi wa matawi ya embe«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=zh1AnvNa6mc&t=408s

Muda: 

00:17:23
Imetengenezwa ndani: 
2015

Imetayarishwa na: 

jfp film

Kupogoa miti ya embe ni muhimu kwa njia kadhaa. Changamoto kubwa ni kujibu maswali kama vile; ni kipi kinapaswa kukatwa, wapi, lini na vipi.

Kimsingi, kupogoa huanza baada ya mti kupandwa na hii huitwa kupogoa kwa mafunzo. Wakati wa kupogoa, kata matawi yanayokua wima yaliyo katikati ili kuunda nafasi ya mzunguko wa hewa na jua kwenye matawi. Pia kata matawi yote ambayo hayasaidii mti kutoa matunda na acha tu matawi yanayotoa matuda. Baada ya kupogoa, ni muhimu kuondoa nyenzo zote zilizokatwa kutoka shambani mwako kwani zinaweza kuoza na hivyo kuvutia wadudu na magonjwa.

Mchakato wa kukata

Ni vyema kuanza kupogoa mti ukiwa ungali mchanga kwa sababu kadiri mti unavyokua bila kukatwa, ndivyo inavyokuwa ngumu kuukata.

Ili kupogoa mti mchanga wa embe, fanya mkato wa kwanza 60 cm hadi 80cm kutoka ardhini. Matawi 4 hadi 6 yatachipuka. Lakini chagua na uache tu matawi 3 hadi 4 kulingana na afya na nguvu ya mti, na pia pembe ambayo matawi yanaibukia. Matawi yanafaa kuwa yanakua katika pembetatu kamili au pembe mraba wakati yakiangaliwa kutoka juu.

Fanya mkato wa pili juu ya chipukizi. Matawi mengine 4 hadi 6 hutokea lakini pia acha tu matawi 3 hadi 4. Hakikisha kwamba hakuna matawi yanayokua katikati ya matawi mengine. Rudia kufanya utaratibu ulio hapo juu ili kukata mara ya mwisho.

Mara tu mti unapopogolewa awali, endelea kufanya upogoaji wa matunzo kila baada ya kuvuna ili kudumisha muundo mzuri wa mti.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0001:52Kupogoa miti ya embe ni muhimu na huanza baada ya mti kupandwa.
01:5303:59Kata matawi yanayokua wima,matawi ya pembeni, na acha tu matawi yanayotoa matuda.
04:0005:20Kushindwa mara kwa mara: Wakulima hukata upande mmoja tu wa mti au hukata matawi mengi sana na hivyo mti huchukua muda mrefu kupona.
05:2107:35Anza kupogoa mapema iwezekanavyo . Baada ya kupogoa, ni muhimu kuondoa nyenzo zilizokatwa kwenye shamba lako.
07:3608:08Iwapo kuna mti mkubwa sana, ukate kabisa na upande mti mpya.
08:0909:33Fanya mkato wa kwanza 60 cm hadi 80cm kutoka ardhini. Matawi manne hadi sita yatatokea, lakini chagua tu 3 au 4.
09:3410:12Kata mkato wa pili juu ya chipukizi. Matawi mengine 4 hadi 6 hutokea lakini pia acha tu matawi 3 hadi 4.
10:1314:07Weka mkato wa tatu kwa vile ulivyofanya awali, na kurudia utaratibu mara nyingine.
14:0814:55Endelea kufanya upogoaji wa matunzo kila baada ya kuvuna ili kudumisha muundo mzuri wa mti
14:5617:23Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *