»Jinsi ya kuondoa Sumu kutoka kwenye Unga wa Muhogo«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://sawbo-animations.org/13

Muda: 

00:02:48
Imetengenezwa ndani: 
2022

Imetayarishwa na: 

SAWBO

Muhogo mchungu una sumu, na unga wake unahitaji kusindikwa vizuri kabla ya kuula. Kula unga wa muhogo uliosindika visivyovyema husababisha upataji wa sumu mara tu baada ya kula.

Chukua unga ambao unataka kupika, na uweke kwenye sufuria au chombo. Sawazisha unga uweke alama ukitumia kisu ili kuonyesha urefu wa unga uliyo kwenye sufuria. kisha ongeza maji safi kidogo kidogo huku ukikoroga mpaka unga utakapokuwa na unyevu kufika kwa kiwango sawa na unga uliyekua kavu awali. Lakini usifanye unga kuwa ma maji zaidi kama uji na haupaswi pia kuwa na mipira ya unga.

Tandaza unga kwenye eneo safi kwa kutumia kijiko au mkono ili unene wake uwe chini ya ule wa kucha ya kidole. Kisha acha unga kwenye jua kwa masaa 2 au kwenye kivuli kwa masaa 5.

Chemsha maji kwenye sufuria na ongeza unga huo hadi utakapopata uzito sawiya.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:47Muhogo mchungu una sumu, na unga wake unahitaji kusindikwa vizuri kabla ya kuula
00:4801:04Ili kuondoa sumu, chukua unga ambao unataka kupika, na uweke kwenye sufuria au chombo. Sawazisha unga na uweke alama kulinga na urefu wake ukitumia ncha ya kisu.
01:0501:19Ongeza maji safi kidogo kidogo huku ukikoroga
01:2001:30Tandaza unga kwenye eneo safi.
01:3101:37Acha unga kwenye jua kwa masaa 2 au kwenye kivuli kwa masaa 5.
01:3801:59Chemsha maji kwenye sufuria na ongeza unga huo hadi utakapopata uzito sawiya
02:0002:48Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *