»Hatua za Uzalishaji wa Mahindi ikijumuisha Utumiaji wa Mbolea ya Majani (Sehemu ya I)«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=cylrrjRdrxs

Muda: 

00:10:01
Imetengenezwa ndani: 
2013

Imetayarishwa na: 

FarmChannelGhana

Mahindi ni zao kuu la chakula na biashara kwa wakulima wengi, hata hivyo kujifunza hatua za uzalishaji na utumiaji wa mbolea ya majani na mbolea ya madini huwasaidia wakulima kuongeza mavuno ya mahindi.

Daima epuka udongo wa kichanga, changarawe na udongo usio na kina kirefu, kwani huzuia ukuaji wa mahindi. Kuna zana nyingi za kupanda mahindi kama vile kisu, na jembe la kuchimba mashimo.

Mchanganyiko wa mbolea za majani na mbolea za madini huongeza mavuno ya mahindi.

Hatua za Uzalishaji

Chagua eneo lenye udongo ulio na rutuba na kina kirefu, na ulime au tumia kemikali kuondoa magugu na kulainisha udongo kabla ya kupanda.

Kisha chagua aina bora ya mbegu ambayo hukomaa ndani ya muda mfupi ili kupata mavuno mengi. Panda katikaka msimu wa upanzi unaopendekezwa.

Pima uotaji wa mbegu ukitumia mbegu zilizoidhinishwa kwa kuhesabu, kupanda na kumwagilia mbegu mia moja zilizothibitishwa.

Panda mbegu kwa kuzingatia matokeo ya vipimo vya uotaji; kati ya 85% – 100% panda mbegu 2, 70% – 84% panda mbegu 3, 50% – 70% panda mbegu 4 au pata mbegu bora, na 0 – 50% pata mbegu mpya.

Panda kwa safu ukizingatia muachano wa 80cm kati ya safu na 40cm ndani ya safu katika kina cha 5–7 cm huku ukitumia zana zinazofaa.

Mbolea za majani na mbolea za madini

Weka mbolea ya NPK yenye uzito wa kilo 100 kwa ekari moja kwa kutengeneza mashimo kwa sentimita 5 kutoka kwenye msingi wa mimea katika wiki ya kwanza.

Katika wiki ya pili, weka 250ml ya kianzio cha mahindi kwa ekari moja, yaani 50ml bomba la kunyunyizia dawa ambalo huchukua lita 15.

Pima kwa ukamilifu 25ml ya kianzio cha mahindi na mimina katika kinyunyizio cha lita 15 kilichojazwa nusu na maji, funga na tikisa vizuri ili kuchanganyika vyema. Kisha jaza bomba na maji.

 

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0001:13Hatua za uzalishaji wa mahindi.
01:1402:13Chagua mahali penye udongo wenye rutuba, usio na maji na ulime au tumia kemikali.
02:1403:08Chagua aina bora ya mbegu na iliyo na kipindi kifupi cha ukomavu.
03:0905:00Panda aina kulingana na msimu unaopendekezwa
05:0106:18Fanya kipimo cha uotaji na uhesabu mbegu zilizoota baada ya siku 7.
06:1907:09Panda mbegu kwa kuzingatia matokeo ya kipimo cha uotaji.
07:1007:36Panda kwa safu ukitumia zana zinazofaa, kwa umbali wa 80cm kati ya safu na 40cm ndani ya safu, katika kina cha 5–7 cm.
07:3707:40Hatua za matumizi ya mbolea ya majani na mbolea ya madini.
07:4107:54Mchanganyiko wa mbolea ya majani na mbolea ya madini huongeza mavuno.
07:5508:37Wiki ya kwanza baada ya kupanda weka 100kg za NPK kwa ekari.
08:3808:50Katika wiki ya pili weka 250ml ya kianzio cha mahindi kwa ekari moja
08:5110:01Pima 25ml ya kianzio cha mahindi, mimina kwenye kinyunyizio cha lita 15, funga na tikisa kwa maji.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *