Dawa za mitishamba dhidi ya uvimbe wa kiwele

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.accessagriculture.org/herbal-medicines-against-mastitis

Muda: 

00:15:12
Imetengenezwa ndani: 
2019

Imetayarishwa na: 

Atul Pagar, Anthra

Uvimbe wa kiwele ni maambukizi au ugonjwa unaofanya kiwele kuwa kigumu na kuvimba, na hivyo ng‘ombe hataki kukamuliwa.

Matumizi ya viuatilifu kwa muda mrefu sio mzuri kwa ng‘ombe. Viuatilifu huathiri maziwa na nyama ambayo sio nzuri kwa matumizi ya binadamu.

Kuzuia

Njia bora ya kuzuia uvimbe wa kiwele ni kudumisha usafi katika zizi la ng‘ombe na eneo la banda la ng‘ombe. Ondoa samadi na chakula kilicho mwagika kwenye zizi. Andaa eneo la kukamua na eneo la kupumzika ili kudumisha usafi.

Osha mikono yako na maji safi kabla na kati ya kukamua wanyama tofauti.

Safisha kiwele kwa maji safi na kukifuta kwa kitambaa safi kabla na baada ya kukamua.

Matibabu

Pima maziwa ya ng‘ombe mara kwa mara, na utibu ng‘ombe mara tu utakapoona dalili za uvimbe wa kiwele.

Kagua ubora wa maziwa. Tumia kifaa cha kukagua uwepo wa uvimbe wa kiwele.

Iwapo utatumia vifa maalum cha kukamua maziwa, tumia plag moja tu kwa kila titi.

Kamua maziwa yote yaliyo kiweleni, laa sivyo viini na vijidudu vinaweza kukua katika maziwa yaliyosalia.

Kufuta kiwele na maji ya uvuguvugu yaliyochemshwa na majani ya mpeera na mwarobaini.

Paka kiwele kilichoathiriwa na mchanganyiko wa kafuri na unga wa samuli kwenye mafuta baada ya kukamua.

Iwapo mnyama hajapata nafuu baada ya kutumia dawa ya mitishamba, basi wasiliana na daktari wako wa mifugo.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:40Dairy farming allows farmers to get income from selling various milk products. Ufugaji wa ng‘ombe wa maziwa huruhusu wafugaji kupata mapato kutokana na kuuza bidhaa anuwai za maziwa
00:4101:27Mastitis is a common disease that infects the udder.Uvimbe wa kiwele ni ugonjwa wa kawaida ambao huathiri kiwele.
01:2802:00Kutumia viuatilifu kutibu uvimbe wa kiwele huathiri uzalishaji wa nyama na maziwa
02:0103:00Dalili: Ugonjwa huo hufanya kiwele kuwa kigumu na kuvimba, na hivyo ng‘ombe hataki kukamuliwa.
03:0003:58Utambuzi: Kagua ubora wa maziwa, Tumia kifaa cha kukagua uwepo wa uvimbe wa kiwele. Iwapo utatumia vifa maalum cha kukamua maziwa, tumia plag moja tu kwa kila titi.
03:5905:05Kudhibiti: Tenganisha eneo la kukamulia na zizi. kudumisha usafi katika zizi la ng‘ombe.
05:0606:42Usafi kwa kukamua: Safisha kiwele kwa maji safi. Kamua maziwa yote yaliyo kiweleni.
06:4307:26Ng‘ombe anafaa kusimama kwa muda wa dakika 40 baada ya kukamuliwa.
07:2708:26Mpe ng‘ombe dawa za mitishamba
08:2711:20Paka kiwele na dawa za kulainisha matiti
11:2113:00Matibabu na dawa ya nyumbani: Tumia majani ya mwarobaini
13:0115:12Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *