Kudhibiti ugonjwa wa bakajani kahawia katika mashamba ya mpunga

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=1Laf3zwRkXk&t=354s

Muda: 

00:14:50
Imetengenezwa ndani: 
2022

Imetayarishwa na: 

Ghana E-Agriculture
Bakajani kahawia ni ugonjwa wa mpunga unaoenezwa kupitia mbegu, na husababisha mavuno duni ukishambulia mashamba na hivyo kusababisha kipato kidogo. 
Ugonjwa huu huathiri mbegu, majani, mashina pamoja na nafaka hivyo kuugundua na kuudhibiti mapema ni muhimu. Bakajani kahawia ni ugonjwa wa ukungu ambao hubadilisha rangi ya majani na husababisha madoa ya kahawia. Bakajani kahawia  kawaida husababishwa na mbinu duni za maandalizi ya ardhi.

Kuenea kwa ugonjwa

Ugonjwa wa bakajani kahawia huenea kupitia mbegu zilizoambukizwa, kwa hivyo inashauriwa sana kutumia mbegu zilizoidhinishwa. Kila wakati hakikisha unatibu mbegu kwa kuziloweka kwenye maji ya uvuguvugu au mchanganyiko wa viuakuvu kabla ya kupanda.

Udhibiti wa ugonjwa

Tayarisha ardhi vizuri kwa kuisawazisha ili kuzuia maji kutuama, na pia ondoa magugu ambayo yanashindana virutubisho vya mimea. Panda kwa kutumia mbegu zilizoidhinishwa kila msimu kutoka kwa wafanyabiashara wa kilimo walioidhinishwa. Ondoa magugu shambani ili kuzuia kuenea kwa magonjwa. Tumia mbolea bora za madini zilizosawaziswa baada ya kuchunguza na kupima rutuba ya udongo ili kuhakikisha ukuaji mzuri wa mazao. Mwagilia mashamba maji na kagua shamba mara kwa mara ili kutambua kwa urahisi mazao yaliyoathirika. Mwishowe, ondoa na uharibu mazao yaliyoathirika, na pia weka dawa za kuua ukungu zilizopendekezwa.
Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:50Bakajani kahawia ni ugonjwa wa mpunga unaoenezwa kupitia mbegu, na husababisha mavuno duni.
00:5101:57Ugonjwa huu huathiri mbegu, majani, mashina pamoja na nafaka hivyo kuugundua na kuudhibiti mapema ni muhimu.
01:5804:47Bakajani kahawia ni ugonjwa wa ukungu ambao hubadilisha rangi ya majani na husababisha madoa ya kahawia.
04:4806:34Ugonjwa wa bakajani kahawia huenea kupitia mbegu zilizoambukizwa
06:3508:40Kila wakati hakikisha unatibu mbegu kwa kuziloweka kwenye maji ya uvuguvugu au mchanganyiko wa viuakuvu
08:4111:48Tayarisha ardhi vizuri kwa kuisawazisha
11:4912:27Panda kwa kutumia mbegu zilizoidhinishwa kila msimu kutoka kwa wafanyabiashara wa kilimo walioidhinishwa.
12:2813:24Ondoa magugu shambani. Tumia mbolea bora za madini zilizosawaziswa baada ya kuchunguza na kupima rutuba ya udongo. Mwagilia mashamba maji
13:2514:50Kagua mashamba mara kwa mara, ondoa na uharibu mazao yaliyoathirika na uweke dawa ya kuua ukungu inayopendekezwa.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *