»Mbolea ya nyungunyungu na mbolea ya minyoo«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=xALvCCq58GI

Muda: 

00:06:05
Imetengenezwa ndani: 
2016

Imetayarishwa na: 

Shramajeevi TV

Kutokana na ongezeko la mahitaji ya bidhaa za kilimo, mbinu mbalimbali za kutengeneza mbolea oza ya kutosha kwa ajili ya kilimo-hai zimebuniwa.

Mbolea ya minyoo ni maarufu sana kwa wakulima wa kikaboni. Kuna aina 2 za minyoo ambao ni pamoja na ule ambao huchimba chini kabisa kwenye udongo na mwingine ambao huishi juu ya udongo. Minyoo ambayo huishi juu ya udongo hula 10% ya udongo na 90% ya nyenzo za kikaboni. Huwa anakula kiwango sawa na uzito wa mwili wake.

Utumizi wa mbolea

Katika ekari moja, kuna kilo 30–40 ya minyoo. Mbolea ya minyoo ina vichocheo kadhaa, na hivyo huifanya kuwa mboji kamilifu. Minyoo pia hukua kutoka kwa mayai, na kutoa mboji. Weka tani 1 ya mboji kwenye vitalu vya mbegu ili kuboresha ukuaji na afya ya miche. Pia ongeza kilo 0.5 za mboji kwa kila mmea wakati wa kupanda na baada ya siku 45. Weka kilo 5–10 za mboji kila mwaka kwa miti mikubwa zaidi. Ongeza maji kwenye matangi ya minyoo na kisha uyakusanye kama mbolea minyoo ya maji. Hii ni mchanganyiko bora wa virutubishi, na vichocheo na hutumika kama kinga nzuri ya wadudu na magonjwa kwenye mazao.

Usindikaji wa mbolea

Minyoo wakubwa asili ya kiafrika hutumiwa. Hawa hustawi kwenye joto la 25–30 na unyevu wa 40–45%. Kisha majani makavu, mabaki ya mazao, makapi ya miwa nakadhalika huongezwa kwenye minyoo. Wakati wa kutekeleza mchakato, epuka kutumia maua ya glyceria na mmea wa tumbaku. Nyunyiza maji na changanya samadi ya ng‘ombe na nyenzo zitakazotumika, kisa weka mchangayiko chini ya kivuli kwa wiki 3–4. Hii kisha hulishwa kwa minyoo.

Jenga paa juu ya matangi ya mboji ya minyoo ili kuzuia mvua na jua ya moja kwa moja. Jenga matanki ukitumia mawe au saruji. Punguza ukubwa wa tanki na toboa tundu chini yalo ili kutiririsha maji ya ziada. Weka safu ya nyenzo zisizo laini chini ndani mwa tanki, na safu ya nyenzo za kikaboni na samadi mbichi ya ng‘ombe juu yake.

Weka safu nyingine ya nyenzo za kikaboni na urudie kutekeleza uratatibu huo hadi tanki litakapojaa. Eneza minyoo juu na umwagilie maji ili kudumisha unyevu. Mbolea huwa tayari baada ya miezi 2–3 kulingana na nyenzo zilizotumika. Kusanya mbolea ya minyoo kutoka juu, na uichuje baada ya kuondoa unyevu wa ziada. Endelea na utayarishaji wa mbolea hii kwa kuongeza nyenzo nyingine kwenye tanki. Jenga sakafu la saruji katika eneo la kutengenezea mboji ya minyoo. Weka mifereji ya maji au majivu karibu na tanki la minyoo ili kudhibiti mchwa. Epuka kutumia viuatilifu.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:19Mbolea ya minyoo ni maarufu sana kwa wakulima wa kikaboni
00:2000:29Kuna aina 2 za minyoo ambao ni pamoja na ule ambao huchimba chini kabisa kwenye udongo na mwingine ambao huishi juu ya udongo.
00:3000:39Minyoo ambayo huishi juu ya udongo hula 10% ya udongo na 90% ya nyenzo za kikaboni.
00:4000:45Katika ekari moja, kuna kilo 30–40 ya minyoo.
00:4600:52Mbolea ya minyoo ina vichocheo kadhaa
00:5301:13Minyoo pia hukua kutoka kwa mayai, na kutoa mboji
01:1401:24Weka tani 1 ya mboji wakati wa kupanda.
01:2501:31Ongeza kilo 0.5 za mboji kwenye vitalu vya mbegu ili kuboresha ukuaji na afya ya miche.
01:3201:40Ongeza kilo 0.5 za mboji kwa kila mmea wakati wa kupanda na baada ya siku 45.
01:4101:46Weka kilo 5–10 za mboji kila mwaka kwa miti mikubwa zaidi
01:4702:12Ongeza maji kwenye matangi ya minyoo na kisha uyakusanye kama mbolea minyoo ya maji.
02:1302:40Minyoo wakubwa asili ya kiafrika hutumiwa. Hawa hustawi kwenye joto la 25–30 na unyevu wa 40–45%.
02:4102:47Majani makavu, mabaki ya mazao, makapi ya miwa nakadhalika huongezwa kwenye minyoo.
02:4802:50Epuka kutumia maua ya glyceria na mmea wa tumbaku.
02:5102:58Nyunyiza maji na changanya samadi ya ng‘ombe na nyenzo zitakazotumika, kisa weka mchangayiko chini ya kivuli kwa wiki 3–4
02:5903:15Lishwa kwa minyoo, ila usiwape nyenzo mbichi..
03:1603:36Jenga paa juu ya matangi ya mboji. Jenga matanki ukitumia mawe au saruji.
03:3703:51Punguza ukubwa wa tanki na toboa tundu chini yalo ili kutiririsha maji ya ziada
03:5204:01Weka safu ya nyenzo zisizo laini chini ndani mwa tanki
04:0204:08Ongeza safu ya nyenzo za kikaboni na samadi mbichi ya ng‘ombe juu.
04:0904:15Weka safu nyingine ya nyenzo za kikaboni na urudie kutekeleza uratatibu huo hadi tanki litakapojaa
04:1604:33Eneza minyoo juu na mboji iliyo na mayai ya minyoo.
04:3404:48Mwagilia maji ili kudumisha unyevu. Mbolea huwa tayari baada ya miezi 2–3.
04:4904:57Kusanya mbolea ya minyoo kutoka juu, na uichuje baada ya kuondoa unyevu wa ziada.
04:5805:07Endelea na utayarishaji wa mbolea hii kwa kuongeza nyenzo nyingine kwenye tanki.
05:0805:20Jenga sakafu la saruji katika eneo la kutengenezea mboji ya minyoo.
05:2105:40Weka mifereji ya maji au majivu karibu na tanki la minyoo ili kudhibiti mchwa.
05:4106:05Muhtasari

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *