Pembejeo za wakulima kama vile mbegu bora huhakikisha mavuno bora na faida kubwa. Miche kutoka kwa mbegu bora huwa na nguvu na hutoa sawa, pamoja na kukua haraka.
Utafiti unaonyesha kuwa kabichi inachukua nafasi ya kwanza ikilinganishwa na sukumawiki. Kilimo cha kabichi nchini Kenya kina soko mbili ambazo ni soko la ndani ya nchi, na soko la nje. Mbegu za Simlaw huhakikisha kuwa wakulima wanapata mbegu bora za kabichi. Kwa hivyo, wakulima wadogo wanaweza kuongeza mavuno yao kwa 20% na kupunguza hasara kwa 30%.
Kilimo cha kabichi
Kabichi hustawi kwenye udongo wa kichanga usiotwamisha maji, na ulio na mboji pamoja na kiwango cha pH cha 6.7 hadi 7.0. Kabichi ni mmea ambao unaweza kustahimili hali tofauti za hewa.
Kuna aina ambayo hustawi vyema katika hali ya hewa ya baridi na wakati aina zingine hustawi katika maeneo ya joto.
Aina mbalimbali za kabichi
Ni muhimu kujua eneo la kilimo ili kutumia aina sahihi ya kabichi. Aina ya Gloria F1 ni maarufu zaidi miongoni mwa wakulima, na hustawi katika maeneo yote ya kilimo.
Matumizi ya mbegu bora ni mojawapo ya vipengele muhimu katika uongezaji wa mazao katika kila mfumo wa kilimo. Upandaji wa aina za kabichi zilizoboreshwa nchini Kenya ni wa juu sana.
Faida za uhandisi wa jeni za urithi
Faida ni pamoja na: ongezeko la mavuno ya mazao, upunguzaji wa gharama za uzalishaji wa chakula au dawa, upunguzaji wa mahitaji ya viuatilifu, uboreshaji wa virutubisho na chakula, ustahimili dhidi ya wadudu na magonjwa.
Ni muhimu kwa wakulima kutumia mbegu ambazo zimepimwa dhidi ya magonjwa na viuatilifu. Upimaji wa udongo ni uchunguzi wa sampuli za udongo ili kubaini viwango vya virutubisho na viini vilivyo udongoni. Pia husaidia kubaini kiwango cha tindikali, madini, maji na viumbe hai ambavyo huboresha afya ya shamba.
Soma zaidi juu ya uzalishaji wa kibiashara na usimamizi wa kabichi -sehemu ya 2.