»Mbinu za kulisha kuku wa nyama kwa bei nafuu na udhibiti wa halijoto«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=vbHQW6wQESY

Muda: 

00:10:45
Imetengenezwa ndani: 
2021

Imetayarishwa na: 

AIM Agriculture

Katika ufugaji wa kuku wa nyama, kutotolesha vifaranga na kulisha ni changamoto kubwa. Mbinu bora katika ufugaji wa kuku husaidia kuongeza tija ya biashara.

Katika usimamizi wa vifaranga, uingizaji wa hewa ni muhimu sana. Tunahitaji kutolea ndege halijoto sahihi na kuondoa hewa mbaya kwa mfano kabonidioksidi, amonia na kabonimonoksidi kutoka kwa banda la kuku. Huku kunatekelezwa kwa kuinua au kushusha mapazia kulingana na hali iliyopo.

Kushughulikia mapazia

Mapazia kwenye eneo la kutotoleshea vifaranga huinuliwa au hushushwa kulingana na tabia za vifaranga na usomaji wa kipima joto. Wakati wa joto, inua pazia ili kuingiza hewa, na wakati wa baridi, inua pazia huku ukiacha nafasi ya takriban sm 15 ili kuruhusu hewa safi kuingia ndani ya banda. Ni makosa kuongeza uingizaji wa hewa kwa kuinua pazia kutoka chini kwenda juu kabisa kwa sababu huku kunaweza kuondoa joto lililokusanywa.

Mkusanyiko wa gesi ya amonia kwenye banda la kuku husababisha harufu mbaya, kuwashwa kwa macho ya kuku, na kuathiri mfumo wao wa kupumua.

Kulisha ndege

Kuanzia siku ya 1 hadi 14, lisha ndege kwa chakula cha kuanzia ambacho kina asilimia 21% ya protini. Chakula hiki kina lishe na husaidia katika ukuaji wa ndege. Kuanzia siku ya 14 hadi 21, lisha ndege wako kwa chakula cha ndege wanaokua. Kutoka siku ya 21 hadi 28 lisha ndege kwenye chakula cha kumalizia. Ni muhimu huruhusu ndege wako kupumzika. Watolee giza ili wapumzike na kusaga chakula.

Kwa siku 5 za kwanza, changanya dawa ya mfadhaiko katika maji ya ndege ili kupunguza mfadhaiko. Hakikisha ndege daima wana maji bora ya kunywa wakati wote.

Kagua shingo ya vifaranga ili kuhisi kama wamelishwa au wamenyweshwa. Ikiwa sehemu hiyo ngumu, jua kwamba kifaranga amekula tu, ikiwa nyororo sana basi kifaranga amekunywa maji tu, na ikiwa inahisi kama uji uji, basi kifaranga amekunywa na kula.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:44Katika usimamizi wa vifaranga, uingizaji wa hewa ni muhimu sana.
00:4502:45Mapazia kwenye eneo la kutotoleshea vifaranga huinuliwa au hushushwa kulingana na tabia za vifaranga na usomaji wa kipima joto.
02:4603:20Madhara ya mkusanyiko wa amonia katika banda la kuku.
03:2103:30Uingizaji hewa usipotekelezwa vizuri huathiri ukuaji wa ndege.
03:3104:00Ndege wanaweza kulishwa chakula kilichochanganywa na mahindi.
04:0105:39Kuanzia siku ya 1 hadi 14, lisha ndege kwa chakula cha kuanzia. Kuanzia siku ya 14 hadi 21, lisha ndege wako kwa chakula cha ndege wanaokua. Kutoka siku ya 21 hadi 28 lisha ndege kwenye chakula cha kumalizia.
05:4006:25Watolee giza ili wapumzike na kusaga chakula.
06:2607:12wa siku 5 za kwanza, changanya dawa ya mfadhaiko katika maji ya ndege ili kupunguza mfadhaiko.
07:1308:04Hakikisha ndege daima wana maji bora ya kunywa wakati wote.
08:0510:00Kagua shingo ya vifaranga ili kuhisi kama wamelishwa au wamenyweshwa.

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *