»Ugonjwa wa kideri, sehemu ya kwanza: dalili na ishara«

0 / 5. 0

Chanzo:

https://www.youtube.com/watch?v=GUuiGHuiPUo

Muda: 

00:09:08
Imetengenezwa ndani: 
2018

Imetayarishwa na: 

AIM Agriculture

Kideri ni ugonjwa wa ndege unaosababishwa na virusi, ambao hauna tiba. Ugonjwa huu huenea kwa haraka sana kutoka kwa ndege walioambukizwa hadi ndege wenye afya ambao hawajachanjwa, na unaweza kusababisha vifo hadi asilimia 100.

Mojawapo ya dalili za ugonjwa wa kideri ni kujipinda shingo na kuyumbayumba katika mwendo. Ugonjwa wa kideri huathiri mfumo mkuu wa mishipa, na hivyo kusababisha ndege kuyumbayumba katika mwendo.

Kupungua kwa uzalishaji wa mayai

Ugonjwa wa kideri huathiri uzalishaji wa mayai. Hupunguza uzalishaji wa mayai, na husababisha na uzalishaji wa mayai yenye kasoro, mayai yenye maganda laini, na mayai yenye maji maji. Pengine, ndege hutaga mayai yasiyo na gamba, na katika hali mbaya ndege hutaga kiwiliwili. Yai la kawaida huwa na kiini chake katikati ya maji, wakati kuku aliye na ugonjwa wa kideri hutaga yai lililo na kiini kilichotenganishwa na maji ya yai.

Dalili zingine

Kutetemeka, udhaifu na kukunja mabawa ni dalili za kawaida katika kuku wa mayai. Viungo vya miguu hupooza. Kwa ndege ambao wamechanjwa awali lakini wameshambuliwa na aina tofauti ya ugonjwa wa kideri, mguu mmoja tu hupooza. Pia miguu yote hupooza kabisa na huonekana kama kijiti kilichokauka.

Ndege hushindwa kutembea ambapo miguu na mabawa yote yamepooza. Ndege pia hushindwa kusimama, kutembea, wala kutumia mabawa.

Mafadhaiko, ambapo ndege huonekana kuwa katika hali ya kukaa na kusinzia kila wakati, huku jicho moja au yote mawili yakifungwa kila wakati.

Kuhema, kukohoa na kuhara. Ndege walioathiriwa na ugonjwa wa kideri kutoa kinyesi cha maji ya kijani kibichi na damu.

Kuanzia dakika ya Hadi dakika y Maelezo
00:0000:36Kideri ni ugonjwa wa ndege unaosababishwa na virusi, ambao hauna tiba, na unaweza kusababisha vifo hadi asilimia 100.
00:3701:15Mojawapo ya dalili za ugonjwa wa kideri ni kujipinda shingo na kuyumbayumba katika mwendo.
01:1604:59Ugonjwa wa kideri hupunguza uzalishaji wa mayai
05:0005:40Ugonjwa wa kideri husababisha na uzalishaji wa mayai yenye kasoro.
05:4106:14Kutetemeka, udhaifu na kukunja mabawa ni dalili za kawaida katika kuku wa mayai.
06:1507:25Viungo vya miguu hupooza.
07:2607:47Ndege hushindwa kutembea ambapo miguu na mabawa yote yamepooza
07:4808:15Mafadhaiko, ambapo ndege huonekana kuwa katika hali ya kukaa na kusinzia kila wakati
08:1609:08Kuhema, kukohoa na kuhara.
09:0909:24Hitimisho

Tazama video ya nje

Kwa kubofya kiunga kifuatacho au kitufe cha kucheza utaondoka kwenye Maktaba ya Video ya FO na utumie tovuti ya nje! Tungependa kukuona tena, kwa hivyo usisahau kurudi!

Soma zaidi

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *